Ijumaa, 3 Februari 2017
Kitu hiki kikubwa kimoja kimekwamisha mafanikio yako
Habari za asubuhi ndugu msomaji wa VIPAUMBELE KWANZA!
Mimi nami namshukuru Mungu wa mbingu na nchi.
Asubuhi hii naomba nikuulize hili swali moja tu: "Kwa nini umekwama jumla
kimafanikio"? Yapo mambo mengi unayoweza kuzungumzia kama vizuizi vya
kufikia mafanikio yako. Na mimi nakubaliana na wewe kuwa vikwazo ulivyo
navyo ni sahihi. Lakini naomba tutajidili kikwazo kimoja kikubwa ambacho ni
uvivu wa kuweka akiba kutoka kwenye pato lako.
Ndugu msomaji huwa unakumbuka kuweka AKIBA kila upatapo pato lako?
Kama unaweka akiba, hongera sana; na kama huweki akiba , amka sasa uanze
kuweka akiba (SAVINGS). Akili isiyojizoesha kuweka akiba inajiandaa kuwa
mtumwa kifedha. Huwezi kukwepa huu ndo uhalisia wenyewe. Nakuomba jitahidi
uwe na AKIBA ya kutosha, hakikisha kila wakati unapopata fedha, anza na akiba.
Save as much as you can for your future. Nikutakie asubuhi njema!
KWA NINI UNASHINDWA KUANZISHA BIASHARA?
Habari za jioni ndugu msomaji wa VIPAUMBELE KWANZA , pole na majukumu ya hapa na pale.
Binafsi sijambo namshukuru Mungu wa Mbinguni.
Jioni hii napenda kuzungumzia kwa nini watu wengi wanatamani kufanya biashara lakini huoni wakifanya hata siku moja. Mimi mwenyewe ni shahidi wa jambo hili. Nina marafiki ninaofanya nao shughuli za kila siku , utawasikia wakizungumzia biashara za kufanya mwisho wa siku unawaona wameahirisha kufanya. Ukiwauliza watakupa sababu za kila namna.
Sababu wanazotoa ni kama:
- Hawana mtaji
- Ni vigumu kupata mtu mwaminifu wa kufanya nao biashara
- Biashara hazitabiriki.
Hizi ni baadhi tu ya sababu za watu wengi kushindwa kufanya au kuanzisha biashara. Huwa najiuliza hawa watu wanataka biashara gani isiyoweza kupata hasara? Unajiuliza hawa watu wanahitaji kweli kufanya biashara au wanatania? Hivyo vyote ni visingizio tu.
USHAURI wangu kwako msomaji: Hata mimi hili jambo limenisumbua miaka michache iliyopita,
nilikuwa najiuliza biashara gani nifanye nitajirike fasta? Ni swali niliwauliza wengi sana, na waliniambia ni ipi japo nilikuja kugundua yafuatayo baada ya muda:
MOJA: Kwa nini watu wengi wanasingizia MITAJI katika kuanza biashara? Mimi nakiri wazi bila unafiki, anayeniambia hana mtaji huwa nakataa huu usemi, kwa sababu; unakuta mtu ana matumizi zaidi ya sh.130, 000/= kwa mwezi halafu ukimtazama ana simu ya laki 1 au zaidi, ukimcheki ana viatu vya gharama. Huyo huyo anakuambia hana MTAJI. Ukweli ni kwamba wengi wanatamani kuanza biashara kubwa kubwa zinazohitaji pesa nyingi. Na kwa sababu hiyo wanaishia kusema mtaji hautoshi na wengine huishia kuchukua mikopo ambayo mwisho wa siku inawaingiza katika madeni. Naomba nikushauri anza biashara ambayo unaweza kuimudi kimtaji. Usilazimishe kuanza biashara kubwa kubwa wakati hata ndogo hujawahi kufanya.
PILI: Kwa nini wengine wanasingizia biashara gani wafanye ya kuwalipa? Napenda kukueleza kuwa biashara zote zinalipa kutegemeana na mazingira biashara ilipo. Ishu sio biashara gani, ishu ni wapi biashara hiyo umeamua kuiweka tegemeana na mahitaji ya jamii. Cha msingi ni kuangalia mazingira, mahitaji ya jamii husika na ufanye utafiti wa kutosha ili ujue changamoto maana zipo. Lakini pia usisahau kuwa hakuna biashara isiyo changamoto.
TATU: Na kwa nini kuna kundi lingine husingizia kuwa UAMINIFU katika biashara ni mdogo. Ni kweli uaminifu ni changamoto inayowakabili wengi. Swali linakuja: Kama uaminifu hakuna au ni mdogo mbona idadi ya wafanya biashara inazidi kuongezeka kila kukicha? Kwa kuwa tunaishi na wanadamu hayo hayana budi kuwepo. Napenda nikiri kuwa huwezi kupata mtu mwaminifu kama unavyotaka, ukimpata ni bahati. Lakini hii haimaanishi kuwa hawapo, waaminifu wapo. Cha msingi ni kujitahidi kusimamia ipasavyo, usije ukamwachia biashara mfanyakazi wako (mwajiriwa). Jitahidi sana kuhakikisha unasimamia angalau kwa kiasi chake. Lakini pia usiogope kuibiwa visenti vidogo vidogo. Muhimu afanye biashara ilete faida.
NNE: Jambo lingine linalokwamisha wajasiriamali wachanga, ni kutokuwa na maandalizi ya kutosha kwa ajili ya malengo yao ya kuanzisha biashara zao. Kwa nini watu wanamatumizi makubwa lakini hawana mitaji? Ni kwa sababu wanakosa NIDHAMU YA PESA. Wanashindwa kuweka AKIBA kwa ajili ya siku zijazo ili iwasaidie kufanya biashara, wanajikuta wanatumia wanachokipata chote. Ukweli ni kwamba fedha yoyote huwa haitoshi, ndiyo maana wanashauri uweke akiba kabla ya matumizi.
TANO: Unapoona pia mtaji hautoshi, jaribu kuangalia watu gani uungane nao ili muunganishe mitaji yenu (kolabo) kwa kiswahili cha mjini. Ungana na wenzako muunganishe mitaji yenu mpate mtaji mkubwa ili muanzishe biashara mnayoitaka. Waswahili husema, KIDOLE KIMOJA HAKIVUNJI CHAWA.
Nawatakia jioni ya fanaka na Mungu awapiganie na kuwapa ujasiri. Zipo sababu nyingi lakini hizi chache zikupe changamoto zaidi. Wako katika VIPAUMBELE KWANZA blogu.
Jumanne, 31 Januari 2017
JE, HUWA UNAJIFUNZA KUTOKANA NA MAKOSA UNAYOFANYA JUU YA FEDHA?
Habari za kuamka ndugu msomaji wa VIPAUMBELE KWANZA! Mimi nimeamka salama namshukuru MUNGU wa Ibrahimu, na Isaka na Yakobo.
Napenda asubuhii tutafakari jambo moja muhimu ambalo kwa sehemu kubwa limetukwamisha tulio wengi hasa katika masuala ya fedha.
Je, huwa unajifunza kutokana na makosa unayofanya juu ya matumizi ya fedha?
Mara nyingi utakuta wengi wengi wanapoona mipango yao ya kimafanikio haipigi hatua hasa katika masuala ya fedha utashangaa kuona anayeanza kulaumiwa ni aidha Serikali, watu wengine au Shetani.
Ushuhuda: Tangu mwaka 2011 na 2012 nimewahi kupata pesa za kutosha katika maisha yangu. Lakini kilichoniumiza zaidi ni kuona sisogei nipo palepale siku zote. Nilijaribu kuwalaumu watu mbalimbali lakini haikutosha na haikunisaidia. Siku moja usiku nikiwa nimelala lilikuja swali akilini mwangu, nalo lilikuwa hivi:
Kwa nini kila siku nina maisha magumu wakati napata pesa nyingi kiasi hiki na wakati sina matumizi mabaya ya fedha? Tatizo liko kwangu au kuna watu wanaonifanyia ubaya ili nitumie fedha isivyostahili? Je, ninawategemezi wengi ? Je, ninaishi kwa kujionyesha kwa watu kama vile nina pesa nyingi? Baada ya kujiuliza maswali mengi kama hayo hapo juu, nilisukumwa kuomba TOBA baada ya kugundua mimi ndiyo chanzo cha tatizo hilo. Nilitambua kuwa, "nilikuwa naishi kwa kujionyesha kuwa nina pesa na kwa sababu hiyo yeyote aliyeniomba pesa nilikuwa nampa. Nikawa najikuta mwisho wa siku sina pesa. Nilipoanza usomaji wa mwandishi mmoja wa kitabu aitwaye DAVE RAMSEY nilipata wazo moja ambalo lilinivusha kwa kiwango kikubwa. DAVE RAMSEY anasema hivi:" Live as a poor in all circumstances while you are SAVING and INVESTING the money you earn". Huyu ndugu anasema hivi:
Ishi kama maskini wakati uo huo ukiwa unaweka AKIBA & na UNAWEKEZA pesa unazopata. Ushauri wangu: Jifunze kutokana naamakosa unayofanya upate kijifunza zaidi kutokana na makosa hayo.
Usikate tamaa unapogundua umefanya makosa katika eneo lolote, dawa ni kujua kwa nini unakosea na kujirekebisha. Nikutakie siku ya fanaka na Mungu awe nawe katika shughuli zako zote, wako katika VIPAUMBELE KWANZA blog.
Napenda asubuhii tutafakari jambo moja muhimu ambalo kwa sehemu kubwa limetukwamisha tulio wengi hasa katika masuala ya fedha.
Je, huwa unajifunza kutokana na makosa unayofanya juu ya matumizi ya fedha?
Mara nyingi utakuta wengi wengi wanapoona mipango yao ya kimafanikio haipigi hatua hasa katika masuala ya fedha utashangaa kuona anayeanza kulaumiwa ni aidha Serikali, watu wengine au Shetani.
Ushuhuda: Tangu mwaka 2011 na 2012 nimewahi kupata pesa za kutosha katika maisha yangu. Lakini kilichoniumiza zaidi ni kuona sisogei nipo palepale siku zote. Nilijaribu kuwalaumu watu mbalimbali lakini haikutosha na haikunisaidia. Siku moja usiku nikiwa nimelala lilikuja swali akilini mwangu, nalo lilikuwa hivi:
Kwa nini kila siku nina maisha magumu wakati napata pesa nyingi kiasi hiki na wakati sina matumizi mabaya ya fedha? Tatizo liko kwangu au kuna watu wanaonifanyia ubaya ili nitumie fedha isivyostahili? Je, ninawategemezi wengi ? Je, ninaishi kwa kujionyesha kwa watu kama vile nina pesa nyingi? Baada ya kujiuliza maswali mengi kama hayo hapo juu, nilisukumwa kuomba TOBA baada ya kugundua mimi ndiyo chanzo cha tatizo hilo. Nilitambua kuwa, "nilikuwa naishi kwa kujionyesha kuwa nina pesa na kwa sababu hiyo yeyote aliyeniomba pesa nilikuwa nampa. Nikawa najikuta mwisho wa siku sina pesa. Nilipoanza usomaji wa mwandishi mmoja wa kitabu aitwaye DAVE RAMSEY nilipata wazo moja ambalo lilinivusha kwa kiwango kikubwa. DAVE RAMSEY anasema hivi:" Live as a poor in all circumstances while you are SAVING and INVESTING the money you earn". Huyu ndugu anasema hivi:
Ishi kama maskini wakati uo huo ukiwa unaweka AKIBA & na UNAWEKEZA pesa unazopata. Ushauri wangu: Jifunze kutokana naamakosa unayofanya upate kijifunza zaidi kutokana na makosa hayo.
Usikate tamaa unapogundua umefanya makosa katika eneo lolote, dawa ni kujua kwa nini unakosea na kujirekebisha. Nikutakie siku ya fanaka na Mungu awe nawe katika shughuli zako zote, wako katika VIPAUMBELE KWANZA blog.
Jumatatu, 30 Januari 2017
FEDHA ILIYO MKONONI MWAKO,
Ndugu msomaji wa VIPAUMBELE KWANZA nakusalimu tena. Pole kwa shughuli za hapa na pale katika kujenga taifa letu.
Jioni hii nitazungumzia jambo moja kubwa nalo ni hili:
MAAMUZI JUU YA FEDHA UNAZOPATA KILA SIKU.
Ndugu msomaji nataka tuzungumzie ukweli juu ya jambo hili linalotukwamisha kila siku.
Swali nalotaka tulijibu wote jioni hii ni : Je, unapokuwa na fedha au pesa mkononi mwako huwa KWANZA unazitumiaje? Naamini kila mmoja wetu huwa ana maamuzi fulani juu ya pesa anazopata kila siku. Watu wengi wanafikiri kwa kuwa wana nguvu (energetic) wakati wanafanya kazi (while working) wanafikiri hiyo hali itaendelea kuwa hivyo. Nasema bila unafiki ndani yangu, siku zinabadilika. Kama makampuni makubwa yanafilisika si jambo la kushanga mtu mmoja akifilisika. Yapo mambo mengi yanayojitokeza hata ambayo hatukuyatarajia katika maisha yetu.
Tuache dhana ya kujisahau eti kwa kuwa napata pesa kila siku basi hakuna shida, huu ni uongo unaofanana na ukweli.
Hivyo ni jambo jema tukaishi kwa kuongozwa na utaratibu fulani katika matumizi ya fedha zinazopita mikononi mwetu. Tusije tukajikuta zimepita hela nyingi sana mikononi mwetu lakini tukajikuta bado tu masikini. Hujawahi kusikia watu wakisema "niliwahi kuwa na hela enzi hizo, sio sasa". Huu si ushuhuda mzuri kwa mwenye malengo mazuri ya kifedha katika maisha yake. Hakuna kitu kibaya unakuta mzazi anakwambia "mwanangu niliwahikuwa na hela kipindi cha ujana wangu usingeteseka hivi", ok ushuhuda kama huu unanisaidia nini mimi mtoto wake? Jibu ni rahisi , "ushuhuda kama huu hauna faida bali hukatisha tamaa maana inaonyesha wazi huyu mtu kuna namna ilitokea pesa ikapotea. Ni afadhali pesa ipotee kwa jambo ambalo ukilisikiliza lina sababu za msingi sio zile mbovu za kutumia pesa kama vile wewe ndo unayezitengeneza.
Pesa inayopita mkononi mwako usipoidharau inaweza kukufanya utajirike hata kama ni ndogo kiasi gani. Kutajirika si suala la wewe unapata pesa nyingi kiasi gani bali ni unaamua nini unapozipata hizo pesa. Unaweza amini kuwa mwenye kipato cha Tsh.300, 000 anajenga nyumba nzuri na mwenye Tsh.700, 000 anashindwa? Jibu ni rahisi na mifano mingi tunayo. Ushauri wangu kwako msomaji:
Unapopata fedha mikononi mwako, KWANZA tulia kabisa, pesa ni yako. Narudia tena, tulia kabisa kama vile huna hela. Baada ya kutuliza akili fanya yafuatayo.
Hatua ya kwanza: Tenga kiasi cha AKIBA kwa ajili ya baadaye. Wataalamu wa masuala ya fedha hutumia neno "pay yourself first". Wakimaanisha jilipe mshahara wako kwanza. Akiba hii usiiguse kabisa ni kwa ajili ya baadaye. Save for yourself for rainy day.
Jambo la pili: Tenga kiasi fulani kwa ajili ya KUWEKEZA.
Kiasi hiki si akiba ni fedha unayoirundika polepole kwa ajili ya kukuza mtaji ili siku utakapohitaji kuanzisha biashara usihangaike sana. Kama unafuatilia uchumi wa dunia unavyokwenda utakuwa unafahamu kuwa kadri siku zinavyokwenda, upatikanaji wa mikopo utakuwa wa masharti sana. Hivyo ni jambo jema sana ukiweza kujijengea nidhamu ya kifedha ili tusitegemee mikopo tu kama chanzo cha mitaji wakati pesa zinazopita mikononi mwetu ni nyingi.
Jambo la tatu: Fedha inayobaki ndo iwe MATUMIZI YALIYO YA LAZIMA.
Kumbuka kuna matumizi holela na matumizi yaliyo vipaumbele. Wengi tukipata fedha tunakimbilia kuweka kwanza matumizi ya kila siku, kisha ndo tunataka kuweka akiba kilichotuzidi. Hii inaweza kutumika kwa wale ambao walishajiweka vizuri kifedha. Kwetu sisi ambao bado tunaelekea kwenye mafanikio ni muhimu sana kufuata hizi kanuni za kifedha, financial management principles.
NB: Sijasema mikopo ni mibaya la hasha! Mikopo ni mizuri ukiitumia vizuri.
Muhtasari:
1. Weka akiba
2. Weka kiasi kwa ajili ya kuwekeza
3. Tenga matumizi yaliyo ya lazima. Kumbuka: Usiweke AKIBA kinachobaki. Haya niliyoyaandika yamenisaidia na mpaka leo nayatumia.
Nawatakia mafanikio mema.
Jioni hii nitazungumzia jambo moja kubwa nalo ni hili:
MAAMUZI JUU YA FEDHA UNAZOPATA KILA SIKU.
Ndugu msomaji nataka tuzungumzie ukweli juu ya jambo hili linalotukwamisha kila siku.
Swali nalotaka tulijibu wote jioni hii ni : Je, unapokuwa na fedha au pesa mkononi mwako huwa KWANZA unazitumiaje? Naamini kila mmoja wetu huwa ana maamuzi fulani juu ya pesa anazopata kila siku. Watu wengi wanafikiri kwa kuwa wana nguvu (energetic) wakati wanafanya kazi (while working) wanafikiri hiyo hali itaendelea kuwa hivyo. Nasema bila unafiki ndani yangu, siku zinabadilika. Kama makampuni makubwa yanafilisika si jambo la kushanga mtu mmoja akifilisika. Yapo mambo mengi yanayojitokeza hata ambayo hatukuyatarajia katika maisha yetu.
Tuache dhana ya kujisahau eti kwa kuwa napata pesa kila siku basi hakuna shida, huu ni uongo unaofanana na ukweli.
Hivyo ni jambo jema tukaishi kwa kuongozwa na utaratibu fulani katika matumizi ya fedha zinazopita mikononi mwetu. Tusije tukajikuta zimepita hela nyingi sana mikononi mwetu lakini tukajikuta bado tu masikini. Hujawahi kusikia watu wakisema "niliwahi kuwa na hela enzi hizo, sio sasa". Huu si ushuhuda mzuri kwa mwenye malengo mazuri ya kifedha katika maisha yake. Hakuna kitu kibaya unakuta mzazi anakwambia "mwanangu niliwahikuwa na hela kipindi cha ujana wangu usingeteseka hivi", ok ushuhuda kama huu unanisaidia nini mimi mtoto wake? Jibu ni rahisi , "ushuhuda kama huu hauna faida bali hukatisha tamaa maana inaonyesha wazi huyu mtu kuna namna ilitokea pesa ikapotea. Ni afadhali pesa ipotee kwa jambo ambalo ukilisikiliza lina sababu za msingi sio zile mbovu za kutumia pesa kama vile wewe ndo unayezitengeneza.
Pesa inayopita mkononi mwako usipoidharau inaweza kukufanya utajirike hata kama ni ndogo kiasi gani. Kutajirika si suala la wewe unapata pesa nyingi kiasi gani bali ni unaamua nini unapozipata hizo pesa. Unaweza amini kuwa mwenye kipato cha Tsh.300, 000 anajenga nyumba nzuri na mwenye Tsh.700, 000 anashindwa? Jibu ni rahisi na mifano mingi tunayo. Ushauri wangu kwako msomaji:
Unapopata fedha mikononi mwako, KWANZA tulia kabisa, pesa ni yako. Narudia tena, tulia kabisa kama vile huna hela. Baada ya kutuliza akili fanya yafuatayo.
Hatua ya kwanza: Tenga kiasi cha AKIBA kwa ajili ya baadaye. Wataalamu wa masuala ya fedha hutumia neno "pay yourself first". Wakimaanisha jilipe mshahara wako kwanza. Akiba hii usiiguse kabisa ni kwa ajili ya baadaye. Save for yourself for rainy day.
Jambo la pili: Tenga kiasi fulani kwa ajili ya KUWEKEZA.
Kiasi hiki si akiba ni fedha unayoirundika polepole kwa ajili ya kukuza mtaji ili siku utakapohitaji kuanzisha biashara usihangaike sana. Kama unafuatilia uchumi wa dunia unavyokwenda utakuwa unafahamu kuwa kadri siku zinavyokwenda, upatikanaji wa mikopo utakuwa wa masharti sana. Hivyo ni jambo jema sana ukiweza kujijengea nidhamu ya kifedha ili tusitegemee mikopo tu kama chanzo cha mitaji wakati pesa zinazopita mikononi mwetu ni nyingi.
Jambo la tatu: Fedha inayobaki ndo iwe MATUMIZI YALIYO YA LAZIMA.
Kumbuka kuna matumizi holela na matumizi yaliyo vipaumbele. Wengi tukipata fedha tunakimbilia kuweka kwanza matumizi ya kila siku, kisha ndo tunataka kuweka akiba kilichotuzidi. Hii inaweza kutumika kwa wale ambao walishajiweka vizuri kifedha. Kwetu sisi ambao bado tunaelekea kwenye mafanikio ni muhimu sana kufuata hizi kanuni za kifedha, financial management principles.
NB: Sijasema mikopo ni mibaya la hasha! Mikopo ni mizuri ukiitumia vizuri.
Muhtasari:
1. Weka akiba
2. Weka kiasi kwa ajili ya kuwekeza
3. Tenga matumizi yaliyo ya lazima. Kumbuka: Usiweke AKIBA kinachobaki. Haya niliyoyaandika yamenisaidia na mpaka leo nayatumia.
Nawatakia mafanikio mema.