Jumapili, 5 Februari 2017

JE! UNAYO MALENGO YA MUDA MREFU?


                   Habari za asubuhi ndugu msomaji wa VIPAUMBELE KWANZA! Natumaini 
                 umeamka salama kabisa. Sifa zirudi kwa Mungu wetu aishiye milele.
                 
                 Asubuhi hii nina swali natamani nikuulize ambalo wengi wetu tunalidharau.
                 Swali lenyewe ni:Je, una malengo ya muda mrefu? 
              Watu wengi kwa kukosa elimu ya kutosha juu ya nidhamu ya 
              fedha, tunafikiri kwa kuwa tuna nguvu na afya na tunaingiza fedha
              kila iitwapo leo, tunadhani mafanikio mazuri hayako mbali. Ni kweli
             ni dhana inayoonekana kuwa sawa, lakini mwisho wa siku hutuweka 
             kweupe kama tuliwekeza kwa muda mrefu au La!

             
             Unaweza kuwekeza maeneo mengi kama vile majengo, ardhi n.k.
             Asubuhi hii naomba tutizame eneo la FEDHA. Ni kweli ninajua
             idadi kubwa ya watu hujiwekea malengo makubwa ya muda mfupi
             na ya muda mrefu. Lakini cha kushangaza ni kuona watu hao hao 
             mwisho wa siku hawana kitu. Kinachowakwamisha ni Utekelezaji tu.
             Malengo ya muda mrefu ni yale ambayo ni zaidi ya miaka 2 na kuen
             delea. 

             Ndugu msomaji, nakushauri kama huna malengo ya muda mrefu 
             anza sasa. Kwa mfano, miaka mitano (5) ijayo unatarajia kupata 
             kitu gani cha ziada kifedha? Sizungumzii kukua kwa biashara yako
             nazungumzia "investing your money to earn for you". Weka pesa 
             sehemu au katika taasisi za kifedha zinazotoa na riba. Haijalishi 
             unapata fedha kiasi gani "wekeza fedha zako" katika taasisi husika 
             , mfano masuala ya hisa (soko la hisa), fanya utafiti ni kampuni gani
            unaweza kuwekeza fedha zako ili zikuzalishie faida huku wewe 
             ukiendelea na mambo mengine. 
             Ngoja nikupe mfano: Kuna rafiki yangu mmoja aliweza kuwekeza 
             sh.50, 000 kila mwezi kwa miaka 5, akaja kuvuna sh.5, 000, 000.
             Miaka 5 si mingi kama unavyofikiria. Kama uongo, nitafute mwaka
             2021 uniambie ulichofanya cha maana zaidi. Mimi huwa naita uwe
             kezaji wa jinsi hii "The magic of Compounding". Invest your money.
             Fikiria ukiweza kuwekeza tsh.150, 000 kila mwezi kwa miaka mitano
             unaweza kupata Tsh.16, 000, 000. Njoo unione baada ya miaka 5 
             uniambie ulichofanya. Ushauri wangu kwako, anza sasa "kuwekeza
            pesa zako hata kama ni kidogo.
           
            Kuna mtaalamu wa masuala ya uwekezaji aitwaye "DAVE RAMSEY"
            anasema hivi "I cannot afford not to Invest my money".
           
           Nikutakie siku njema!   

0 maoni:

Chapisha Maoni