Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo UCHUMI. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo UCHUMI. Onyesha machapisho yote

Alhamisi, 6 Aprili 2017

Praise the Lord!
I am very glad to contact you once more, it is just the unfailing love of Jesus Christ on us. It is not because we deserve, no!
   Dear brother/sister in Jesus, I would like to post this essential realm in our life of what have we to do to achieve financial freedom according to God's plan..
You are warmly welcome!

1. Transfer Ownership to God
      The saved must transfer ownership of every possession to God. This means money, time, material possessions, education, even earning potential for the future. This is essential to experience the spirit-filled life in the area of finances (See Psalms 8:4-6).
      
    We must realize that there no substitute for this step. If we believe that we are the owners of even a single possession, then the events affecting that possession are going to affect our attitudes. God will not force His will on us. He will not input His perfect will into our lives unless we first surrender our wills to Him.
  
However, if we make a total transfer of everything to God, He will demonstrate His ability. It is important to demonstrate and accept God's conditions for His control (Deut 5:32-33). God will keep His promise to provide every need we have through physical, material, and spiritual means, according to His perfect plan.

It is simple to say that we will make a total transfer of everything to God, but it is not so simple to do. At first, we will experience some difficulty in consistently seeking God's will in the area of material things, because we are so accustomed to self-management and control. But financial freedom comes from knowing God is in control. 
What a great relief it is to turn our burdens over Him. Uhuru wa kifedha kibiblia . Then, if something happens to car, we can say, "Father, I gave this car to You; I 've maintained it to the best of my ability, but I don't own it. It belongs to you, so do with it whatever you would like, "Then look for the blessing God has in store as a result of this attitude.
Transfering your possessions to God does not mean taking all you possess to your church but if Holy Spirit leads and directs you there do to accordingly.
   
The next method will be "how to become Dept Free" biblically. Have a nice life and much blessing!

HOW CAN WE ACHIEVE BIBLICAL FINANCIAL FREEDOM?

Jumatatu, 27 Machi 2017

JIUNGE NA VIPAUMBELE KWANZA.



MAFANIKIO NI KUWA NA VIPAUMBELE BORA

* indicates required







Bwana Yesu apewe sifa!
Ndugu msomaji wa makala nazotoa kila wiki, nimesukumwa leo ndani yangu kukushirikisha kitu kifuatacho ambacho kila aliye wa Bwana anapaswa kuwa nacho katika moyo wake! Ni kweli kila mtu anatamani kuwa na fedha nyingi, lakini kuna swali huwa hatujiulizi, nalo ni hili: Nataka fedha nyingi kwa ajili ya nini? Hili ni swali zuri sana tunalopaswa kujiuliza kila wakati, kwa sababu unaweza ukawa unapata fedha kisha zinakujeruhi, kwani hujawi kusikia kuwa kuna ndoa zinakufa fedha zinapoongezeka? Kuna watu wanafikiri kuwa ukishakuwa na fedha, basi wewe ni mbarikiwa! Mimi nakataa usemi huu, kidunia ni usemi sawa, lakini Kibiblia au Kimungu si usemi sahihi hata kidogo. Kuna watu wakipata fedha, dhambi zinapata nafasi mioyoni mwao, na wengine mpaka zinawanjia heshima. Ndiyo maana ni muhimu, wale walio wa Bwana Yesu, tumtafute kwa bidii ili atawale mali zetu ndipo tutakuwa salama.
Uhuru wa kifedha ni nini Kibiblia?
Dondoo ya 1:
Ni wakati tabia ya moyo wako haitawaliwi na kuwepo au kutokuwepo kwa fedha bali itawaliwe na Roho Mtakatifu, katika neno la Mungu la Biblia.
     -Ukisoma Mathayo 6:21, maandiko yanatuambia mahali hazina (fedha) ya mtu ilipo, ndipo na moyo wa huyo mtu ulipo. Kwa mantiki hii, fedha ina nguvu kuliko moyo wa mtu. Na fedha ikiwa na nguvu kuliko moyo wako, bado hujawa na uhuru wa kifedha ule Mungu anaoutaka. Hivyo ni muhimu tukabidhi vyanzo vyetu vya fedha au mapato kwa Mungu kwa njia ya maombi, ili Roho Mtakatifu atawale nguvu iliyomo ndani ya fedha ili kuusaidia moyo wako usitawaliwe na fedha.

Dondoo ya 2:
Uhuru wa kifedha ni wakati unaweza kufanya chochote kile ambacho Mungu anataka ufanye bila kukwamishwa na kutokuwepo kwa fedha.
-Ni muhimu kwa watu wa Mungu kumtegemea Mungu katika mambo ambayo Mungu anataka wafanye. Una vitu vingapi moyoni mwako ambavyo unajua kabisa ya kuwa Mungu anataka uvifanye lakini kiwango cha fedha ulichonacho kinakukwamisha? Kwa mfano; semina za neno la Mungu, kujiendeleza kimasomo, kupanua biashara yako, au kubadilisha kazi ulinayo au kuchangia gharama za kazi ya Mungu katika kanisa au huduma mbalimbali.
    Umewahi kujiuliza nani huwa anaamua hayo mambo niliyoyataja hapo juu yatekelezwe vipi-ni moyo wako au fedha uliyonayo?
Kwa watu wengi kinachoamua ni fedha waliyonayo halafu mioyo yao inafuata uamuzi wa fedha zao!
Je! moyo wako una nguvu ya kuikataa fedha unayopewa kwa masharti yasiyo mazuri kama msaada au mkopo-na bado mipango yako ikatekelezeka na hali ya uhuru wako wa kiroho ukaendelea kuwa mzuri?

Dondoo ya 3:
Ni wakati mapato yako yanapokuwa ni makubwa kuliko mahitaji na matumizi yako ya kila siku-bila kudhoofisha hali yako ya kiroho. (Wafilipi 4:19)
"Na Mungu wangu atawajazeni kila mnakihitaji kwa kadri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu".Njia mojawapo anayoitumia Mungu kukujaza na kila unachokihitaji ni fedha-maana imeandikwa, "......fedha huleta jawabu la mambo yote" (Mhubiri 10:19). Ikiwa na maana, Mungu anaweza kutumia fedha kujibu au kukupa jawabu la mahitaji yako.
Ikiwa ni hivi basi, uhuru wa kifedha kwako utakuwa pia na maana ya kuwa, Mungu anapotumia fedha kukupa jawabu la mahitaji yako, usihamishe imani yako toka kwa Mungu na kuiweka kwa fedha. Au usihamishe imani yako toka kwa Mungu na kuiweka kwenye kazi, mradi, kampuni, huduma, biashara, sadaka au mtu unayemtegemea sana bali imani yako ibaki kwa Mungu, haleluya!
Zipo maana nyingi za uhuru wa kifedha kibiblia, lakini hizi chache, zikupe changamoto ya kupanuka zaidi juu ya jambo hili. NB: Weka imani yako kwa Mungu uwe na fedha nyingi au kidogo. Fedha zinaweza kutumiwa na Mungu kukupa jawabu la hitaji lako, lakini Mungu apewe nafasi ya kwanza moyoni mwako.
Wiki ijayo tutaangalia njia za kibiblia zinazoweza kutusaidia kupata uhuru wa kifedha.
Mungu akubariki, mshirikishe na mwingine ujumbe huu! 

NAMNA YA KUPATA UHURU WA KIFEDHA KIBIBLIA

Ijumaa, 24 Machi 2017

Bwana Yesu asifiwe rafiki! Tumsifu Yesu Kristo!
Ndugu msomaji wa VIPAUMBELE KWANZA nachukua nafasi hii kukupa pole kwa majukumu uliyonayo pamoja na changamoto unazopitia. Hayo hayana budi kuwepo maadamu bado tunaishi katika dunia hii. Lakini nikutie moyo kuwa kila jambo lina majira yake.

           Ndugu msomaji, uwe mkristo usiwe mkristo sisi wote Mungu anapenda kutufanikisha. Yesu hakuwafia wakristo bali alikufa kwa ajili ya ulimwengu na wewe ukiwemo. Kuna maswali ambayo watu tumekuwa tukijiuliza mara kwa mara bila majibu. Na kwa kuwa dunia hii ina wasomi wengi tumefika mahali tumemwekea Mungu wetu mipaka. Hivyo tumeamini wapo watu tukiwaeleza matatizo tuliyo nayo yataisha, lakini tunakuja kukumbuka kuwa bado yanajirudia kwa kuwa bado hatujapata ufumbuzi wake halisi. 
 Swali ambalo limekuwa likinisumbua kwa miaka mingi ni hili: Kwa nini watu wanaomwamini Mungu hawafanikiwi kiuchumi wakati Bwana Yesu ameahidi kutufanikisha? Je, neno la Biblia ni neno la Mungu kweli au ni kitabu tu cha kihistoria? Kama Mungu anatupenda si atupatie mafanikio sisi tulio watoto wake?
       Siku moja nilikuwa natafakari juu ya jambo hili, wakati natafakari nikawa nasoma huu mstari katika Biblia " Mathayo 6:33, Bali utafuteni kwanza Ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa". 
Niliendelea kutafakari huu mstari kwa muda mrefu sana, baada ya muda nikaona kitu ambacho kilibadilisha maisha yangu kiroho na kiuchumi hatua kwa hatua. Andiko hili linasema hivi, Tafuta kwanza Ufalme wa Mungu, Biblia haisemi, Omba kwanza ufalme wa Mungu Uje, no! no! no! Biblia inasema tafuta. Tafuta..haisemi, Omba Ufalme wa Mungu uje, hapana..
Wakati naendelea kuwaza kwa kina juu ya mstari huu, nikasikia wazo moyoni mwangu..watu wengi wanafikiri kutafuta ufalme wa Mungu ni kuokoka au kuzaliwa upya mara ya pili kwa Roho Mtakatifu, lakini si hivyo. Kutafuta Ufalme ni kusoma neno la Mungu kwa msaada wa Roho wa Mungu na kwa maombi, huku ukimuuliza Mungu unachotaka. Wakati naendelea kutafakari hili wazo lililokuwa ndani yangu, nikakumbuka ule mstari wa Hosea 4:6 usemao, "Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa..
Ndugu msomaji, fahamu jambo hili katika maisha yako, katika nyakati hizi za mwisho, kila mtu anataka kufanikiwa hasa kiuchumi, na ni jambo zuri, lakini tamaa hii haitufikishi popote. Tunapata pesa nyingi, lakini zinapotea bila maelezo, tunaanza upya. Tunajitahidi hata kufuata ushauri tunaopewa na wataalamu wa masuala ya kifedha lakini bado tunakwama. Sikia na uelewe, kama unataka kuona Mungu akikufanikisha, huna budi kujua na kufuata misingi/kanuni zilizoko katika Ufalme wa Mungu katika neno lake. Kuwa mtoto wa Mungu tu haitoshi kufanikiwa kiuchumi mpaka utakapojua misingi iliyo katika neno lake na kuitenda, haleluya!
Jambo la kukumbuka ni hili, Unataka kufanikiwa ili ufanye nini na hayo mafanikio?
Kwa sababu Mungu akikufanikisha anataka aliweke imara AGANO LAKE. Ikiwa kusudi lako la kufanikiwa si kuimarisha Agano la Mungu, sahau mafanikio Kimungu ("Bali utamkumbuka Bwana, Mungu wako, maana ndiye atupaye nguvu za kupata Utajiri; ILI ALIFANYE IMARA AGANO LAKE alilowapa baba zako, kama hivi leo" (Kumbukumbu la Torati 8:18).
Ukisoma vizuri maandiko matakatifu kwa msaada wa Roho Mtakatifu, utagundua kuwa bado kuna mambo mengi hatujayajua na kwa sababu hiyo, tunapoyatenda hatupati tunachotaka kwa kuwa hatuyaelewi vizuri tunayatumia isivyo (misapplication of holy scriptures). Soma pia nafasi ya mwanamke kibiblia

Ndugu msomaji naomba Mungu akupe ufahamu na afungue macho yako ya ndani uone kile Mungu anachotaka uone katika neno lake. Pia nikushauri jambo hili, jizoeze kujiombea kwa Mungu ili akupe kulijua neno lake swasawa na jinsi anavyotaka ujue, na ukishajua tenda kile neno linataka. Hili somo litakuwa na mwendelezo kwani ni somo refu sana.
Na usisahau kuniombea ikikupendeza kwani hatuwezi kuandika haya mambo bila msaada wa Mungu. 
Karibu tufuatane pamoja katika utangulizi huu!
Ukurasa wa 1.
  • Ni kusudi la Mungu kutufanikisha. 
 Ukisoma Waefeso 5:17, Utagundua jambo lifuatalo;
Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana.
Ukirudi nyuma mstari wa 16, utagundua kwa nini amesema 'kwa sababu hiyo'..Sababu ipi?
Verse 16. Zamani hizi ni za uovu, na ule wa 15, unasema, tuenende kama watu wenye hekima, hekima hii inapatikana katika neno lake.
Maandiko yanasema, tusiwe wajinga, kwa hiyo tujitahidi kuyajua mapenzi ya Bwana (will of the Lord). Hivyo amini moyoni mwako kuwa Mungu anao mpango wa kukufanikisha.
Ukisoma Waefeso 5:14, maandiko yanatuambia, Amka wewe usinziae....na Kristo atakuangaza.

Jambo la 2: Tafuta Ufalme wa Mungu na haki yake.
Ukisoma (Mathayo 6:33), Biblia inasema, Tafutaeni kwanza ufalme wa Mungu, na haki yake, na hayo yote, mtazidishiwa. Tunapaswa kutafuta kujua makusudi ya Kimbingu juu ya hicho tunachoomba tupewe. Tunatafutaje? (a) Kwa njia ya neno lake
(b) Kwa kumuomba Mungu huku tukimuuliza. Maana ukisoma Isaya 45:11, Niulize.....
Laiti watu wa Mungu tungefuata kile neno linachotushauri, nina uhakika tungetambua ukuu wa Mungu..Je, tunayajua mapenzi ya Mungu katika shughuli zetu na biashara zetu? Je, huwa tunautanguliza ufalme wa Mungu

Jambo la 3: Amini moyoni mwako kuwa Mungu anafurahia mafanikio yetu (watoto wake).
Soma Zaburi 35;27; Mathayo 7:11,....Biblia inasema, japokuwa sisi tulio waovu tunajua kuwapa watoto wetu vipawa vyema, je, Yeye Mungu asiye muovu si zaidi sana anatamani kutufanikisha zaidi? Oo..haleluya!
Sikia mtu wa Mungu, acha kumlaumu Mungu wetu, eti anatupa umaskini ili tunamwabudu, si kweli na haipo katika neno lake, Mungu hatuonyi kwa kutumia umaskini bali kwa kutumia neno lake...

Jambo la 4: Mpango wa Mungu kwetu ni kuwa na vingi tele. Soma Warumi 12:2, Yohana 10:10.
Mungu anavyo vitu vingi na utajiri mwingi na anatamani atupe hivyo vitu..Kumbuka kuwa Mungu anavyo vitu vyote na anatamani atufanikishe kwa kadri ya alivyo navyo...
Hagai 2:8, Mwanzo 15:5. 

Jambo la 5: Jua uhusiano uliopo kati ya Mungu, Neno la Mungu, na wewe (Mimi).
God, His word and You.

 

JE, UNAZIJUA KANUNI ZA UFALME WA MUNGU KATIKA KUKUFANIKISHA?

Jumapili, 12 Machi 2017




JE UNATAKA MABADILIKO KIFEDHA? FANYA JAMBO HILI KWANZA TU

* indicates required







Habari za Leo rafiki yangu? Ni matumaini yangu kuwa unaendelea vizuri. Yawezekana unapitia changamoto mbalimbali katika maisha yako. Japokuwa unapitia yote hayo jipe moyo mkuu, kwani kila lenye mwanzo lina mwisho.
Leo napenda nikushirikishe jambo hili muhimu moja tu unalopaswa kulikumbuka kila siku. Kabla ya kukueleza hili jambo moja; hebu tujiulize haya maswali. Lengo la kujiuliza haya maswali ni kutokana na mitazamo ya watu juu ya mafanikio yao kiuchumi.
Watu wamekata tamaa utadhani maisha ndo basi. Wengine wakikumbuka wingi wa pesa zilizopita mikononi mwao wanaishiwa nguvu kabisa. Ukweli ni kwamba mafanikio yako hayatokani na pesa unazotengeneza/unazopata bali maamuzi unayochukua juu ya hizo fedha bila kujali kiwango cha pesa ulichonacho. Ndugu msomaji, acha kukata tamaa, acha kujilaumu, acha kunung'unika, cha msingi fanya jambo moja kwanza tu, hayo mengine hayana budi kuja. 
Muhimu ni kujizoeza kuwa na subira, maana mafanikio ya kweli yanahitaji muda mrefu hasa kwa wale ambao ndo wanavuta kasia. Usiwaone matajiri wa leo hawakuanza leo bali wanamuda mrefu.
Yapo mambo mengi ya kujifunza sana juu ya mafanikio na uchumi. Kadri tutakavyopata nafasi tutazidi kujadili mambo ya kuzingatia ili tuweze kuvuka mahali tulipokwama.Soma pia
TRIANGLE FINANCIAL PRINCIPLES

Kabla ya jambo hilo tujiulize maswali yafuatayo:
1. Unapata fedha kiasi gani kwa siku?
2. Una wategemezi wangapi wanaokutegemea?
3. Ni vizuizi gani vilivyokuzuia usifikie malengo yako?
4. Ni lini umejipanga kutoka kwenye umaskini?
5. Ni mkakati gani uliouandaa kukutoa hapo ulipo katika mafanikio yako ya kifedha?

Ndugu rafiki unayesoma somo hili, hapo juu umejiuliza hayo maswali 5, mengine utajibu wewe mwenyewe, mimi nitajibu hili la 4 na 5 tu.

Ukiona mtu yeyote asiyejiuliza maswali katika yanayomhusu si rahisi kutoka mahali alipo.
Swali la 4 linasumbua sana watu waliowengi wanaweka malengo yao bila kuhusianisha na muda, na kwa sababu hiyo wanakosa uvumilivu na hamasa ya kusubiria hicho wanachokitaka. Naomba nikushauri kuwa kila lengo unaloweka liwekee muda wake.

Katika swali la 5, tumejiuliza kuwa ni lazima tuwe na mkakati thabiti wa kutusaidia kufikia malengo yetu. Kila mmoja wetu anapaswa kuwa na njia au utaratibu wa uhakika sio wa kusadikika. Leo nataka nikukumbushe njia au utaratibu huu mmoja tu.
Jiwekee utaratibu wa kuwekeza fedha zako kila unapopata pesa. Ziwe nyingi au kidogo. Kwa mfano, fungua account bank inayotoa riba na kila mwisho wa mwezi weka (mfano 50,000 tshs) ila usiombe ATM CARD. Ngoja nirudie tena, tafuta taasisi inayoaminika na inayotoa riba nzuri, fungua akaunti na anza kuweka fedha kidogo kidogo kila mwezi, na fanya hivyo kwa muda mrefu kama miaka 5 hadi 10. Nakueleza ukweli ukiweza hili umeweza kufanikiwa. Jambo hili ukilifanya huna budi kutoka ulipokwamia na utashangaa hata wewe mwenyewe. Zipo taasisi kama UTT Amis au EXIM BANK wanazo hizi huduma. Ila ningekushauri uanze kuwekeza UTT Amis kwani wana riba nzuri. Sikulazimishi ila hapo ndipo na mimi ninapowekeza!
Uvumilivu ni muhimu lakini wazungu husema, "Investing is the magic financial compounding" wakimaanisha kuwa, uwekezaji ni mfumo unaokulipa kwa kushangaza mno.
Nikutakie utekelezaji mwema, wako kocha na mjasiriamali Faustin Mahende, nipigie simu kwa namba zifuatazo:
+255 765 977 026
facebook: Mlishi Mahende
Twitter: Mlishifaustin@Mlishifaustin.   

FANYA JAMBO HILI KWANZA TU

Jumamosi, 11 Machi 2017

Karibu tena ndugu msomaji wa VIPAUMBELE KWANZA!
Najua umechoka na shughuli za hapa na pale za siku ya leo. Pole sana rafiki. Katika usiku huu naomba nikufikirishe jambo moja tu la muhimu kwetu. Ukitazama muda kimwaka (kwa kuangalia urefu wa mwaka utadhani hutazeeka. Hata mimi nilikuwa nawaza sana juu ya hili, lakini ukitizama muda kidakika au kimasaa, utagundua tuna siku chache sana. Kama mwaka una siku 365, bado ni chache sana. Hivyo ni bora tukaanza kujiandaa tutakavyoishi kifedha. Kumbuka kuwa utakapokuwa mzee hutakuwa na nguvu za kufanya kazi tena kama mwanzo, lakini pia usiweke sana tumaini kwa watoto wako hata kama umewasomesha, kwani wanaweza kukukwamisha. Hivyo ili kujiandaa ipasavyo nakushauri ufanye mambo makubwa mawil. Lakini usisahau, tunazungumzia kifedha.

Moja, anza kuwekeza fedha zako kwa taasisi zinazotoa riba nzuri kwa muda mrefu kama miaka 5 au zaidi. Kila fedha unayopata usisahau kutenga sehemu ya kuwekeza.

Pili, hakikisha una kitega uchumi kizuri kitakachokuwa kinakuzalishia fedha wakati wewe huna nguvu tena.

Nikutakie usiku mwema rafiki yangu, na Mungu akulinde. 

UMEJIANDAA KWA KIASI GANI KIFEDHA UTAKAPOKUWA MZEE?

Jumatatu, 6 Machi 2017

Habari za Jumatatu rafiki yangu! 
Naamini unaendelea vizuri na harakati za kujikwamua kimaisha kila siku. Leo nataka nikushirikishe jambo moja muhimu nalo ni "kiwango cha maisha ya mtu kinatokana na kiwango cha mawazo yake". Huu ni ukweli usiopingika ukiamua kujifanyia tathmini wewe mwenyewe. Kwa lugha nyingine, yale anayoyawaza mtu ndiyo atakayoyatenda na kuyaishi. Kuna msemo usemao, "you are what you eat". Hata kimawazo, mtu anaishi kwa kutekeleza mawazo anayoyaona kuwa kwake ni sahihi. Mawazo ni nini? Mawazo kwa tafsiri isiyo rasmi ni mtazamo alionao mtu juu ya jambo fulani au kitu fulani na kuamini kuwa ndivyo kilivyo.
 Mawazo haya yanatoka wapi?
Mawazo yanayomwongoza mtu yanatokana na vyanzo vingi. Yanaweza kutokana na anapokuwa anajifunza jambo. Kwa mfano, mtoto ukimwambia kuwa usipokuwa msafi utapatwa na magonjwa mbalimbali, mtoto huyo atapata mtazamo mpya ndani yake kuwa uchafu huleta magonjwa, na akilifanyia kazi wazo hilo ndivyo atakavyoishi.

Chanzo kingine cha mawazo ni yale anayoyasikia na kuyaamini kuwa ndivyo 
yalivyo.
Mtu huyu ataanza kutekeleza katika maisha yake yale yote aliyoyasikia na ndivyo atakavyoishi.

Chanzo kingine ni yale anayoyasoma kwenye maandiko mbalimbali yawe ya kidini au ya kawaida.
Ndiyo maana kwa urahisi zaidi angalia misimamo ya watu juu ya imani za dini zao. Hawa watu wanaishi na kutekeleza kile kilichoandikwa na ndiyo maisha yao yanakuwa katika wigo wa kile wanachokiamini.
Kwa mfano niliwahi kusikia mtu mmoja akisema kuwa kufanya kazi kwa bidii ni kutokuwa na imani, huyu mtu kamwe hawezi kuishi kwa kujishughulisha katika maisha yake.

Hivyo muonekano wa nje wa mtu ni matokeo ya yale anayoyawaza ndani yake. Kwa mfano siku moja nikiwa kazini kwangu tulikuwa tunabishana na wafanyakazi wenzangu juu ya utajiri na umaskini.
Swali lililoibua mjadala lilikuwa hivi:
"Kitu gani kinamfanya mtu mmoja awe tajiri na mwingine awe masikini? Je hawa watu wamepangwa na Mungu waishi hivi?
Hili ndilo swali lililoibua mjadala. Watu waligawanyika pande mbili zinazopingana, upande wa kwanza wanaamini kuwa, ukiwa masikini ujue umeumbwa uwe hivyo tena walisimamia mstari wa Biblia wa "Mithali 22:2, unaosomeka hivi:Tajiri na maskini hukutana pamoja; Bwana ndiye aliyewaumba wote". Ni kweli ukitazama haraka huu mstari unaweza ukakubaliana nao, lakini ukitafakari kwa kina hutakubaliana nao, kwa kuwa wao wanauelewa isivyo. Nasema hivyo kwa sababu ukisoma 2Wakorintho 8:9, Biblia inasema hivi: "Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake".
Ukisoma vizuri hapa utaelewa kuwa Yesu alipokuja duniani na Ufalme wake mabegani mwake, mojawapo ya vitu alivyokuja kufanya ni kugongomelea laana ya umaskini msalabani, ili sisi tuwe matajiri. Alibeba umaskini tuliokuwa nao ili tupate neema upya ya kuwa matajiri.
Baada ya andiko hili mjadala ulipamba moto, ikabidi niwapeleke kwenye maandiko haya, Isaya 48:17 " Bwana Mkombozi wako, Mtakatifu wa Israeli, asema hivi; Mimi ni Bwana, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye katika njia ikupasayo kuifuata".
Baada ya andiko hili wakasema tumekuelewa kwa kiasi fulani. Kwa nini walinielewa? Kwa sababu Biblia haijipingi, bali inafafanua jambo kwa vifungu vingi, ndiyo maana si vizuri kusimamia mstari mmoja.
Kama Mungu ndiye atupaye nguvu ili tupate faida, inawezekanaje wengine awaumbe maskini? 
Ukisoma kwa kingereza andiko walilosimamia utaelewa vizuri, maana inasema, maskini na tajiri wote waliumbwa na Mungu na wanaishi wote katika dunia hii moja. Biblia haijasema, ALIWAUMBA MASKINI NA MATAJIRI. Sasa tuyaache hayo turudi kwenye somo letu. Baada ya hapo waliniuliza hivi:
Sasa wewe unafikiri ni kwa nini iwe hivyo?
Niliwajibu hivi: Utofauti wa maisha yetu ni kuwa na FIKRA TOFAUTI juu ya namna ya kufanikiwa. Niliwaeleza kuwa vile unavyojua kitu ndivyo unavyokifanya si zaidi ya hapo. Kama umefundishwa baiskeli huwezi ukaendesha gari bila kujifunza gari. Niliendelea kuwaambia hivi, akili ya mtu ili iweze kuishi vizuri lazima ipate mafundisho sahihi. Niliwapa mfano, mtoto ukimfundisha "kuhesabu" 1, 2, 3, 4....ukamwacha. Hawezi akajua kusoma moja kwa moja (automatically) kwa kuwa tu anajua kuhesabu. Lazima pia afundishwe kusoma ndipo ataweza kusoma. 
Vivyo hivyo na watu wazima kuna vitu tusipofundishwa hatuwezi kuvijua. Ndiyo maana wasomi kuwa maskini si suala la kushangaza, kwa kuwa mifumo ya elimu ya nchi nyingi hazimuandai mtu kufanikiwa kimaisha bali zinamuandaa mtu awe mtaalamu wa kile anachosomea tu. Hivyo ili msomi naye afanikiwe inabidi apate mawazo mapya yanayohusu mafanikio. Ndiyo maana na kuna mtu ukimpa mil30 bado ataendelea kuwa maskini pamoja na kuwa na hela zote hizo.
Mimi mwenyewe kuna siku nilikuwa natafuta kitu kwenye GOOGLE nikakutana na neno linasema hivi:
Learn to save in whatever little you earn. Kwa mara ya kwanza nilianza safari ya kuweka akiba. Lakini nilikuwa nikiweka akiba najikuta nimeitumia. Siku moja nikakuta kitabu kimeandikwa, the decision you take on the money in your hand, can make you rich or poor.
Baada ya kusoma hicho kitabu maisha yangu na mtazamo wangu juu ya pesa umebadilika kiasi fulani.
Ushauri wangu kwako. Jifunze na jizoeze kusoma vitabu mbalimbali vinavyohusu mafanikio unayohitaji. Lakini uwe mwangalifu na vitu unavyosoma, maana kuna falsafa nyingine ambazo ukitaka kuweka kwenye matendo vitu haviendi. La msingi mwombe Mungu akusaidie kabla hujasoma kitabu au makala yoyote maana si vyote ni vya kusoma. Kuna maandiko unaweza ukasoma na maisha yako yakawa mabaya.
Tumia muda wako kujifunza zaidi kwani akili yako inahitaji kupata maarifa mapya. Kumbuka hivyo ulivyo ndivyo unavyowaza ndani yako.
Nakutakia kila laheri rafiki yangu. Wako mwandishi na refarii wa VIPAUMBELE KWANZA.
 
 



 

MAISHA YAKO YANATOKANA NA UNAVYOWAZA NDANI YAKO

Ijumaa, 3 Machi 2017

Habari za asubuhi rafiki yangu!
Binafsi sijambo, namshukuru Mungu.
Leo nataka tujifunze namna ya kuchukua maamuzi sahihi tunapochukua MIKOPO (LOANS) katika kufanya biashara na matumizi mengine.

Ndugu msomaji wa mtandao huu; nina uhakika unajua kuwa mwanadamu maadamu yu hai hana budi anahitaji kuwa na fedha awe mkubwa au mdogo, awe tajiri au masikini, wote tunahitaji fedha. Huu ndio ukweli wa mambo.
Na katika uhitaji huu, uchumi wa dunia umekuwa ukijifunza na kufanya tafiti nyingi juu ya kuhakikisha kila mtu ili aweze kufanya biashara lazima ahitaji pesa au hela au fedha. Na kwa sababu hiyo, benki nyingi na taasisi mbalimbali duniani zimeanzisha mfumo wa kukopesha na kurudisha faida (riba) kwa aliyekukopesha fedha hizo (loan).

Ndugu rafiki yangu, shida imekuja pale wakopaji wanapojidanganya wakidhani mkopo ni msaada au huduma ya kusaidia wasiojiweza. Namaanisha nini?
Namaanisha kuwa unapokopeshwa fedha ujue aliyekukopa, anahitaji na RIBA katika fedha hiyo, upate hasara au upate faida lazima umrudishie fedha zake pamoja na RIBA. Na si kosa kumpatia RIBA mkopeshaji kwani anafanya biashara. 
Riba ni faida utakayomzalishia kwa kipindi maalumu mnachokubaliana kimkataba.
Nachotaka ufahamu ni hiki, aliyekukopa anafanya biashara na wewe, na ukiwa mzalishaji bora unakuwa mwaminifu kwa aliyekukopa.
Zingatia jambo hili: MKOPO ni BIASHARA.
Kwa kuwa siku hizi kumekuwa na ukosefu wa mitaji, taasisi mbalimbali za kifedha zilizo rasmi na zisizo rasmi zimeanzisha huduma za mikopo tena kwa urahisi zaidi, na kadri siku zinavyoendelea, huduma hii ya mikopo inazidi kupamba moto.
Na wahitaji kwa kutokujua hili, wamechangamkia FURSA hizi bila kujiuliza maswali, na hali zao za maisha wengine zimeyumba jumla. Sisemi kwa kukuogopesha, nasema ili ufanye maamuzi mazuri katika masuala ya mikopo.

Natamani nikushauri jambo moja kubwa! Siku zote unapochukua mkopo jiulize maswali yafuatayo:
1.Mkopo huu unatolewa na taasisi ipi?
Si watu wengi sana wanaotafuta mikopo wanajiuliza swali hili, wao wanachotaka ni hela tu, mengine baadaye! Kuwa mwangalifu juu ya hili. Unapotaka kukopa, fuatilia kutaka kujua hiyo taasisi ikoje. Ndiyo maana wengine wameumizwa jumla na wameporomoka kimaisha kwa sababu ya mahali walipochukua mikopo. Nakumbuka mwaka fulani, kuna taasisi walianzisha mfumo fulani, ukitaka mkopo, unatoa hela za kwako kwanza, wao wanakuambia kuwa, inabidi uwekeze kwanza kwao kisha baada ya muda wao watakukopesha fedha za kukutosha. Na kwa kuwa unakuwa na kiu ya fedha, unajikuta umetoa fedha zako. Ndugu msomaji, na mwaka huo watu wengi walitoa fedha zao na mpaka leo, hiyo taasisi ilikopotelea hakujulikani. 
Kumbuka kuwa, kuna uhusiano wa karibu kati ya fedha na hali ya kiroho ilikotoka fedha hiyo. Na hiyo roho itafuatilia hizo fedha. Ndiyo maana kuna sehemu ukikopa fedha huzifanyii chochote hata kama umejiandaa kufanya kitu fulani. Ukishazipata tu, akili inafanya kinyume, baada ya fedha kuisha ndipo unashtuka. Ikiwezekana unakopa tena na tena, mwisho wake, unaishia pabaya.
muhimu: Fanya uchunguzi wa kina wa mahali unataka kukopa fedha.

2. Unajua RIBA ya mkopo unaotaka kuchukua?
Ni muhimu na ni lazima uulize wahusika juu ya RIBA zao, na wanakokotoaje hizo riba. Waulize hizo riba ni kwa mwaka au kwa mwezi? Waulize usiwaogope, maana kuna wengine wakifika sehemu hizo utadhani wao ni malaika, waulize vizuri, ukiridhika sawa, usiporidhika achana nao, hiyo ni biashara sio huduma. Kwa mfano, unaweza ukaambiwa riba ni 1.6% , halafu wewe huulizi unajua riba nafuu. Au unafikiri nakutania? Wako watu wengi wamechukua mikopo bila kujua utaratibu wa riba.
muhimu: fahamu kwa undani utaratibu wa riba zao.

3. Je, naruhusiwa kufuta mkopo nje na muda tuliopatana?
Watu wengi hawaulizi swali hili muhimu sana, wao kwao kinachotafutwa ni fedha. Ndugu msomaji, waulize hivi: Naweza kuja kurudisha au kulipa fedha zenu hata kama ni kabala ya muda wa kimkataba? Waulize tena hivi: Mtu anapokuja kufuta mkopo wake, mnatoa riba au hamtoi? Na unapojibiwa waombe vipeperushi au maandiko yanayodhihirisha hayo. Usipende kuambiwaambiwa kwa mdomo tu. Omba kupewa nyaraka.
Lakini pia unaweza ukawauliza: Je, ikatokea nikafa, mkopo wangu utafutwa au waliobaki watawajibika nao? Omba kufafanuliwa vizuri. Kufa kupo maadamu unaishi chini ya jua.
Swali la mwisho, waulize hivi: Ikatokea nimekwama kifedha, naweza kusimamishiwa mkopo kwa muda fulani? Waulize wala usiogope!

4. Jiulize hili swali mwenyewe, "kwa nini nataka kuchukua mkopo?
Ndugu msomaji ni muhimu ujue jibu la swali hili, kwani mkopo ni fedha ya mtu amekupa uizalishe upate faida na mgawane hiyo faida. Ndiyo maana ni muhimu ujue kuwa mkopo ili uweze kumpatia faida yake mkopeshaji na wewe upate faida yako, huna budi kuizalisha. Kuna msingi mmoja wa fedha nao ni huu:Fedha huwakimbia wasiojua kuizalisha.
Usichukue mkopo kufanyia mambo ya ovyo hovyo wakati huna hata kitega uchumi kingine!
Wapo watu wanashangaza mno, wao ilimradi fedha zipo yeye atazichukua tu.

ushauri wangu kwako, usianze kuchukua mkopo mkubwa kwa mara ya kwanza, anza na kidogo ili ujue uwezo wako. Mkopo ni sawa na bunduki ya kuwindia wanyama, ukiitumia vizuri, unampata mnyama huyo, ukiitumia vibaya, unakugharimu wewe mwenyewe.

Nawatakia Jumamosi njema na baraka tele!
 

KWA NINI UNAHITAJI MKOPO?

POLENI WOTE KWA MAJUKUMU!
Mchana huu naomba ujiulize hili swali moja tu
Nifanye nini ili nitoke kwenye hii hatua ya maisha?

TAFUTA JIBU LA SWALI HILI MOJA TU

Ijumaa, 24 Februari 2017

Ndugu msomaji wa VIPAUMBELE KWANZA umeamkaje siku ya leo? Ni matumaini yangu kuwa umeamka mapema kabisa na harakati za kupambana na maisha ya kila siku. Leo hii napenda nikushirikishe jambo moja muhimu. 
Je! umejiandaa vya kutosha kuishi katika mafanikio ya kiuchumi miaka 5 ijayo yaani 2023. Umejiwekea malengo gani ya kuhakikisha unakuwa na uchumi mzuri kufikia mwaka 2023? Siku moja nilimuuliza hili swali rafiki yangu nayefanya naye kazi mahali fulani akaniambia hivi, "Faustine huwezi kuweka malengo ya miaka mingi hivo, akaendelea kusema, "una uhakika gani kuwa mwaka 2023 utakuwa hai? Mimi kwanza nilimshangaa na nilishtuka sana, nilitegemea angeniambia, ondoa mashaka. Huu ndio ukweli halisi, watu wengi hasa vijana wa kizazi hiki, kweli wanatafuta fedha na wanapata, cha ajabu mno, wanazitumia ovyo hovyo, mwisho wa siku wanajikuta hawana kitu. Wengi wanajitahidi wananunua mashamba na viwanja ni vizuri sana. Lakini swali langu liko pale pale, wamejiandaaje kifedha miaka hiyo ijayo? Ndugu msomaji unayesoma makala hii, inawezekana umeshajijenga, Mungu akuinue zaidi, lakini pia inawezekana bado unapambana, ningekushauri ujitahidi kuwa na malengo mahususi ya kimkakati na yanayotekelezeka. Ili uweze kujiandaa vizuri fanya jambo hili moja tu kwanza.
ANZA KUWEKEZA FEDHA ZAKO KIDOGO KIDOGO .
Narudia tena anza kuwekeza fedha zako kidogo kidogo kwa watoao riba. Nina uhakika baada ya muda utaanza kuona mafanikio kwako. Ngoja nikupe mfano mzuri.
Kuna rafiki yangu mmoja alinitangulia kikazi, yeye alivyoanza kazi yake alipata bahati ya kuwa na siri hii muhimu. Akatafuta taasisi nzuri akawekeza fedha zake kwa miaka 5 tu. Alijinyima akaanza kuweka (deposit) Tsh.50,000 kila mwezi kwa miezi 60 au miaka 5. Akajikuta ana Tsh.499,645.19 ambayo ukikadiria ni karibu Sh.5, 000, 000. Akapata mtaji wa kuanzia biashara. Hivi leo tunavyoongea yuko mbali kimaisha. Unaweza ukasema, anafanya kazi, ni sawa, lakini ukipiga mahesabu yako vizuri utagundua kuwa, sh.50, 000 kwa mwezi ni sawa na sh.1300 kwa siku. Ubaya ni kwamba, vijana walio wengi siku hizi wanatumia fedha zao kwa fujo wakidhani kuwa wataendelea kuwa nazo. Si kweli usijidanganye, maisha yanabadilika, miili yetu inachoka. Ifike mahali fedha nazo zitufanyie kazi. Unataka kuniambia huwezi pata sh. 1000 tu kwa siku ukaiweka kando? Kama huwezi angalia unatumia shilingi ngapi kwenye vocha ya simu na mawasiliano kwa mwezi. Nakushauri jitahidi usiishi kama BOSS wakati bado hujafikia uhuru wa kutosha wa kifedha. Acha kutapanya pesa, kumbuka una wategemezi wengi hapo baadaye. Na kama tayari unao wategemezi, basi huna budi kutulia na kujipanga vema. 
Ndugu msomaji, mwaka juzi kuna kundi la watu 7 waliungana wakawa wanaungana kwa kuweka sh. 50,000 kila mwezi kila mmoja. Hivyo wanachanga sh.350, 000 na wameamua kufungua biashara fulani mwaka 2021, kwa mahesabu ya haraka hawatakosa mil.48. Hii ni nguvu ya uwekezaji. Nakutakia siku njema! 

UMEJIAANDAJE KIUCHUMI MIAKA 5 IJAYO?

Jumatatu, 20 Februari 2017

Ndugu msomaji wa VIPAUMBELE KWANZA habari za mchana? Binafsi namshukuru Mungu sijambo!
Mchana huu naomba tuzungumzie jambo moja kubwa ambalo linazidi kuvuruga watu, nalo ni Uchumi (economics). Ndani ya uchumi kuna BIASHARA na masuala ya FEDHA. naomba kwa sasa nizungumzie upande wa FEDHA.
Kwa nini watu wanalalamika kila kukicha kuwa uchumi ni mgumu? Maisha ni magumu, wengine uongozi wa nchi ni mbaya hivyo umepelekea ugumu wa maisha. Unaweza ukaendelea kulalamika lakini hakutakusaidia hata kidogo.
Unalopaswa kujua ni hili: Mafanikio ya maisha yako ni wewe mwenyewe!
Watu wengi wanajua kuzalisha fedha, lakini idadi kubwa wanashindwa kujua kuwa kupata fedha nyingi iwe toka kwenye biashara au kazi hakutakufanya uwe tajiri hata siku moja. Ngoja nirudie tena! "Making more money every day does not make you rich! Tufahamu kuwa kuna tofauti ya kuingiza pesa nyingi na kufanikiwa sana. Ndiyo maana huwezi kushangaa kukuta mwenye kipato cha Tsh. 300, 000 kwa mwezi akiwa na mafanikio makubwa kuliko mwenye kipato cha Tsh.600, 000 kwa mwezi. 
Utofauti wao ni mtazamo wao wa kifikra juu ya misingi ya fedha. Ndugu msomaji umejiandaaje kuhakikisha unakuwa na mafanikio makubwa kiuchumi?

Hebu tujibu maswali yafuatayo:
1. Una vipaumbele katika maisha yako?
2. Una malengo ya muda mrefu katika maisha yako?
3. Ni lini umejiandaa kuingia kwenye orodha ya wenye mafanikio?
4. Ufanye nini ili utoke mahali ulipokwama kiuchumi?

Kama una vipaumbele jitahidi kuvitekeleza na kuhakikisha unafikia makusudi yako juu ya hivyo vipaumbele. Kama huna jitahidi uwe navyo, maana bila vipaumbele huwezi kuona mafanikio, sahau! Usiishi kama mbayuwayu, kumbuka tumeletwa duniani kwa makusudi fulani na baada ya muda sisi tunapita. 
Ngoja nikufikirishe jambo moja la muhimu: Siku moja nilikaa chumbani nikiwa na fedha mkononi mwangu, nikajiuliza swali lifuatalo: " Miaka 5 ijayo nitakuwa na umri wa miaka mingapi? Na katika umri huo natakiwa niwe nimeshafanya kipi na kipi? Je, watoto wangu watakapofikia umri X watakuta mazingira gani ya kiuchumi? Nilikaa kwa muda nikajisikia kutetemeka ndani yangu. Nilikumbuka fedha zilizopita mkononi mwangu, nikatoa machozi. Nilijiuliza jambo moja , nifanyeje ili niweze kufikia malengo yangu?
Siku moja nilikuwa nasoma makala moja iliyoandikwa na mzungu mmoja nikakuta neno hili "being poor is a decision and being rich is a decision too"
Maana yake "kuwa maskini ni uchaguzi na kuwa tajiri ni uchaguzi pia".
Baada ya kusoma hii sentesi nilijisikia vibaya sana nikajua huyu mzungu anadharau maskini. Lakini baada ya siku kadhaa nilimtembelea kaka yangu mmoja nikamuuliza hivi: Wengine wanafanyeje mpaka wanafanikiwa? Je, kuna ambao Mungu amewapangia kuwa masikini na wengine kuwa matajiri? Kaka akanijibu, hapana! Tofauti ya wanaofanikiwa na wasiofanikiwa ni kuwa wanaofanikiwa wanajua misingi ya fedha na wasiofanikiwa hawaijui. Akaendelea kusema hivi; "watu wengi wanafikiri kwa kuwa wana nguvu na wanaingiza fedha wanafikiri watakuwa matajiri automatically, lakini sivyo. 
Wakati naendelea kujifunza juu ya jambo hili nilibahatika kupata makala moja ambayo ilibadilisha maisha yangu.
Kama unataka kuona unaishi maisha ya uhuru wa kifedha fanya mambo yafuatayo: 
1. Hakikisha unajiwekea akiba.
Ndugu msomaji, haijalishi unapata fedha kiasi gani, tenga akiba kwanza kabla hujafanya matumizi yoyote. Watalaam wa fedha wanashauri angalau 15% ya pato lako liwe akiba.

2. Wekeza
Ndugu msomaji haijalishi unapata fedha nyingi au ndogo, wekeza fedha yako kwa watoao riba. Tafuta taasisi au kampuni nzuri na wekeza fedha zako huko. Wekeza kwa muda mrefu ndipo utaweza kupata faida kubwa. Hivyo, tenga kiasi kingine cha fedha kwa ajili ya kuwekeza.

3. Hakikisha una vitega uchumi zaidi ya kimoja.
Mifereji mingi ya fedha ni ya muhimu sana kwani mfereji mmoja ukikauka bado utaendelea vema kuliko kutegemea huo mmoja tu.

4. Uwe mtoaji (giving) kwa watu.
Utoaji ni kanuni moja ya kiroho ambayo ni ya muhimu sana kwa mwanadamu. tujitahidi kuwabariki wengine hicho tunachopata kwani kwa kupitia kwao tunapata zaidi wanapomtukuza Mungu. Huwezi kupokea kama hutoi.

kwa leo tuishie hapa. Somo lijalo tutaangalia hizi njia namna ya kufanya ili uweze kufikia malengo yako. Kila la heri rafiki yangu msomaji, wako master wa VIPAUMBELE KWANZA. Mungu akuzidishie kwa kila ulifanyalo.     

MAAMUZI UNAYOCHUKUA JUU YA PESA UNAZOPATA YANAWEZA KUKUFANYA UWE TAJIRI AU MASKINI

Jumapili, 19 Februari 2017

Ndugu msomaji wa VIPAUMBELE KWANZA habari za kuamka? 
Ni matumaini yangu kuwa umeamka salama kabisa japo changamoto kwa mwanadamu 
hazikwepeki awapo chini ya jua.
 Muhimu ni kujipa moyo kwani aliyekuumba yuko pamoja na wewe kila hatua. ya maisha yako.
        Ndugu msomaji wa VIPAUMBELE KWANZA miongoni mwa vitu ambavyo vimekuwa vikikwamisha wafanya biashara na wajasiriamali ni MADENI YASIYOKOMA. Ni kweli kuwa na deni sio kitu cha kushangaza sana lakini kuwa na deni lisilo la lazima ni jambo la kushangaza.
  Ukweli ni kuwa MADENI (DEPTS) yana athari sana kwa mdaiwa hasa anaposhindwa kuyalipa.
Hivi ulishawahi kudaiwa? Kama umewahi au bado unadaiwa ni muda mwafaka wa kukataa kuingia kwenye madeni yasiyo ya lazima. Wengi huwa wananiambia kuwa haiwezekani kuishi bila deni, ukifikiri jambo hili kishabiki utadhani falsafa hii ni kweli. Lakini nakiri kuwa inawezekana kutoingia kwenye madeni yasiyo lazima kama utaamua kutoka katika kifungo hicho.

Naomba tujibu swali hili kila mmoja akijitathmini: Je! ni kwa nini kila siku najikuta katika madeni?
Nitajibu swali hili kijumla (in general) kwa kuwa kila mmoja wetu anazo sababu za kwake..
Nakiri wazi kuwa zipo sababu nyingi mno zinazotufanya kujikuta katika vifungo vya madeni (FINANCIAL BONDAGE) sugu. Baaadhi ya sababu hizo ni hzi zifuatazo:
  • KUTOJIWEKEA AKIBA YA KUTOSHA
  • KUISHI MAISHA YA KUIGA
  • KUWA NA CHANZO KIMOJA CHA MAPATO
  • KUTOZINGATIA MATUMIZI YA BAJETI 
  • KUWA NA WATEGEMEZI WENGI KIFEDHA
  • KUCHUKUA MIKOPO BILA MAANDALIZI
Hizo ni baadhi tu ya sababu zinazotunyima uhuru wa kifedha (FINANCIAL FREEDOM).
Hakuna kitu kinanitesa kama DENI katika maisha haya. Deni ni adui wa fikra na hutuweka utumwani kwa yule au wale wanaotudai. Hivyo hatuna budi kuwa waangalifu katika matumizi ya fedha tunazopata kila siku. 
Endelea kufuatilia makala nazoandika ili upate kujifunza mambo mengi juu ya uchumi na jinsi unavyoweza kufanikiwa. Kila jambo linaanza na maamuzi. Hatuwezi kufikia UHURU WA KIFEDHA mpaka tuwe huru na madeni yaani tusiwiwe na watu. Kibaya zaidi ukiwiwa na mtu asiye na hekima utajuta. Hivyo nitakueleza njia zilizonisaidia kutoka kwenye madeni.
Karibu tuendelee kujifunza pamoja mambo mbalimbali yanayohusu maisha na mafanikio.
Wako master wa VIPAUMBELE KWANZA. Kila heri rafiki. 

JE! UMESHINDWA KUTOKA KWENYE MADENI?

Ijumaa, 3 Februari 2017

Habari za jioni ndugu msomaji wa VIPAUMBELE KWANZA , pole na majukumu ya hapa na pale.
Binafsi sijambo namshukuru Mungu wa Mbinguni.
Jioni hii napenda kuzungumzia kwa nini watu wengi wanatamani kufanya biashara lakini huoni wakifanya hata siku moja. Mimi mwenyewe ni shahidi wa jambo hili. Nina marafiki ninaofanya nao shughuli za kila siku , utawasikia wakizungumzia biashara za kufanya mwisho wa siku unawaona wameahirisha kufanya. Ukiwauliza watakupa sababu za kila namna. 
        Sababu wanazotoa ni kama: 
  1. Hawana mtaji
  2. Ni vigumu kupata mtu mwaminifu wa kufanya nao biashara
  3. Biashara hazitabiriki.
Hizi ni baadhi tu ya sababu za watu wengi kushindwa kufanya au kuanzisha biashara. Huwa najiuliza hawa watu wanataka biashara gani isiyoweza kupata hasara? Unajiuliza hawa watu wanahitaji kweli kufanya biashara au wanatania? Hivyo vyote ni visingizio tu.

USHAURI wangu kwako msomaji: Hata mimi hili jambo limenisumbua miaka michache iliyopita,
nilikuwa najiuliza biashara gani nifanye nitajirike fasta? Ni swali niliwauliza wengi sana, na waliniambia ni ipi japo nilikuja kugundua yafuatayo baada ya muda:

MOJA: Kwa nini watu wengi wanasingizia MITAJI katika kuanza biashara? Mimi nakiri wazi bila unafiki, anayeniambia hana mtaji huwa nakataa huu usemi, kwa sababu; unakuta mtu ana matumizi zaidi ya sh.130, 000/= kwa mwezi halafu ukimtazama ana simu ya laki 1 au zaidi, ukimcheki ana viatu vya gharama. Huyo huyo anakuambia hana MTAJI. Ukweli ni kwamba wengi wanatamani kuanza biashara kubwa kubwa zinazohitaji pesa nyingi. Na kwa sababu hiyo wanaishia kusema mtaji hautoshi na wengine huishia kuchukua mikopo ambayo mwisho wa siku inawaingiza katika madeni. Naomba nikushauri anza biashara ambayo unaweza kuimudi kimtaji. Usilazimishe kuanza biashara kubwa kubwa wakati hata ndogo hujawahi kufanya. 

PILI: Kwa nini wengine wanasingizia biashara gani wafanye ya kuwalipa? Napenda kukueleza kuwa biashara zote zinalipa kutegemeana na mazingira biashara ilipo. Ishu sio biashara gani, ishu ni wapi biashara hiyo umeamua kuiweka tegemeana na mahitaji ya jamii. Cha msingi ni kuangalia mazingira, mahitaji ya jamii husika na ufanye utafiti wa kutosha ili ujue changamoto maana zipo. Lakini pia usisahau kuwa hakuna biashara isiyo changamoto. 

TATU: Na kwa nini kuna kundi lingine husingizia kuwa UAMINIFU katika biashara ni mdogo. Ni kweli uaminifu ni changamoto inayowakabili wengi. Swali linakuja: Kama uaminifu hakuna au ni mdogo mbona idadi ya wafanya biashara inazidi kuongezeka kila kukicha? Kwa kuwa tunaishi na wanadamu hayo hayana budi kuwepo. Napenda nikiri kuwa huwezi kupata mtu mwaminifu kama unavyotaka, ukimpata ni bahati. Lakini hii haimaanishi kuwa hawapo, waaminifu wapo. Cha msingi ni kujitahidi kusimamia ipasavyo, usije ukamwachia biashara mfanyakazi wako (mwajiriwa). Jitahidi sana kuhakikisha unasimamia angalau kwa kiasi chake. Lakini pia usiogope kuibiwa visenti vidogo vidogo. Muhimu afanye biashara ilete faida.

NNE: Jambo lingine linalokwamisha wajasiriamali wachanga, ni kutokuwa na maandalizi ya kutosha kwa ajili ya malengo yao ya kuanzisha biashara zao. Kwa nini watu wanamatumizi makubwa lakini hawana mitaji? Ni kwa sababu wanakosa NIDHAMU YA PESA. Wanashindwa kuweka AKIBA kwa ajili ya siku zijazo ili iwasaidie kufanya biashara, wanajikuta wanatumia wanachokipata chote. Ukweli ni kwamba fedha yoyote huwa haitoshi, ndiyo maana wanashauri uweke akiba kabla ya matumizi.

TANO: Unapoona pia mtaji hautoshi, jaribu kuangalia watu gani uungane nao ili muunganishe mitaji yenu (kolabo) kwa kiswahili cha mjini. Ungana na wenzako muunganishe mitaji yenu mpate mtaji mkubwa ili muanzishe biashara mnayoitaka. Waswahili husema, KIDOLE KIMOJA HAKIVUNJI CHAWA. 
Nawatakia jioni ya fanaka na Mungu awapiganie na kuwapa ujasiri. Zipo sababu nyingi lakini hizi chache zikupe changamoto zaidi. Wako katika VIPAUMBELE KWANZA blogu.  


KWA NINI UNASHINDWA KUANZISHA BIASHARA?

Jumanne, 31 Januari 2017

Habari za kuamka ndugu msomaji wa VIPAUMBELE KWANZA! Mimi nimeamka salama namshukuru MUNGU wa Ibrahimu, na Isaka na Yakobo. 
     Napenda asubuhii tutafakari jambo moja muhimu ambalo kwa sehemu kubwa limetukwamisha tulio wengi hasa katika masuala ya fedha.

Je, huwa unajifunza kutokana na makosa unayofanya juu ya matumizi ya fedha?
Mara nyingi utakuta wengi wengi wanapoona mipango yao ya kimafanikio haipigi hatua hasa katika masuala ya fedha utashangaa kuona anayeanza kulaumiwa ni aidha Serikali, watu wengine au Shetani. 
Ushuhuda: Tangu mwaka 2011 na 2012 nimewahi kupata pesa za kutosha katika maisha yangu. Lakini kilichoniumiza zaidi ni kuona sisogei nipo palepale siku zote. Nilijaribu kuwalaumu watu mbalimbali lakini haikutosha na haikunisaidia. Siku moja usiku nikiwa nimelala lilikuja swali akilini mwangu, nalo lilikuwa hivi:
Kwa nini kila siku nina maisha magumu wakati napata pesa nyingi kiasi hiki na wakati sina matumizi mabaya ya fedha? Tatizo liko kwangu au kuna watu wanaonifanyia ubaya ili nitumie fedha isivyostahili? Je, ninawategemezi wengi ? Je, ninaishi kwa kujionyesha kwa watu kama vile nina pesa nyingi? Baada ya kujiuliza maswali mengi kama hayo hapo juu, nilisukumwa kuomba TOBA baada ya kugundua mimi ndiyo chanzo cha tatizo hilo. Nilitambua kuwa, "nilikuwa naishi kwa kujionyesha kuwa nina pesa na kwa sababu hiyo yeyote aliyeniomba pesa nilikuwa nampa. Nikawa najikuta mwisho wa siku sina pesa. Nilipoanza usomaji wa mwandishi mmoja wa kitabu aitwaye DAVE RAMSEY nilipata wazo moja ambalo lilinivusha kwa kiwango kikubwa. DAVE RAMSEY anasema hivi:" Live as a poor in all circumstances while you are SAVING and INVESTING the money you earn". Huyu ndugu anasema hivi:
Ishi kama maskini wakati uo huo ukiwa unaweka AKIBA & na UNAWEKEZA pesa unazopata. Ushauri wangu: Jifunze kutokana naamakosa unayofanya upate kijifunza zaidi kutokana na makosa hayo. 
Usikate tamaa unapogundua umefanya makosa katika eneo lolote, dawa ni kujua kwa nini unakosea na kujirekebisha. Nikutakie siku ya fanaka na Mungu awe nawe katika shughuli zako zote, wako katika VIPAUMBELE KWANZA blog.

JE, HUWA UNAJIFUNZA KUTOKANA NA MAKOSA UNAYOFANYA JUU YA FEDHA?

Jumatatu, 30 Januari 2017

 Ndugu msomaji wa VIPAUMBELE KWANZA nakusalimu tena. Pole kwa shughuli za hapa na pale katika kujenga taifa letu.
Jioni hii nitazungumzia jambo moja kubwa nalo ni hili:
MAAMUZI JUU YA FEDHA UNAZOPATA KILA SIKU.
Ndugu msomaji nataka tuzungumzie ukweli juu ya jambo hili linalotukwamisha kila siku.
         Swali nalotaka tulijibu wote jioni hii ni : Je, unapokuwa na fedha au pesa mkononi mwako huwa KWANZA unazitumiaje? Naamini kila mmoja wetu huwa ana maamuzi fulani juu ya pesa anazopata kila siku. Watu wengi wanafikiri kwa kuwa wana nguvu (energetic) wakati wanafanya kazi (while working) wanafikiri hiyo hali itaendelea kuwa hivyo. Nasema bila unafiki ndani yangu, siku zinabadilika. Kama makampuni makubwa yanafilisika si jambo la kushanga mtu mmoja akifilisika. Yapo mambo mengi yanayojitokeza hata ambayo hatukuyatarajia katika maisha yetu.
       Tuache dhana ya kujisahau eti kwa kuwa napata pesa kila siku basi hakuna shida, huu ni uongo unaofanana na ukweli.

Hivyo ni jambo jema tukaishi kwa kuongozwa na utaratibu fulani katika matumizi ya fedha zinazopita mikononi mwetu. Tusije tukajikuta zimepita hela nyingi sana mikononi mwetu lakini tukajikuta bado tu masikini. Hujawahi kusikia watu wakisema "niliwahi kuwa na hela enzi hizo, sio sasa". Huu si ushuhuda mzuri kwa mwenye malengo mazuri ya kifedha katika maisha yake. Hakuna kitu kibaya unakuta mzazi anakwambia "mwanangu niliwahikuwa na hela kipindi cha ujana wangu usingeteseka hivi", ok ushuhuda kama huu unanisaidia nini mimi mtoto wake? Jibu ni rahisi , "ushuhuda kama huu hauna faida bali hukatisha tamaa maana inaonyesha wazi huyu mtu kuna namna ilitokea pesa ikapotea. Ni afadhali pesa ipotee kwa jambo ambalo ukilisikiliza lina sababu za msingi sio zile mbovu za kutumia pesa kama vile wewe ndo unayezitengeneza. 
Pesa inayopita mkononi mwako usipoidharau inaweza kukufanya utajirike hata kama ni ndogo kiasi gani. Kutajirika si suala la wewe unapata pesa nyingi  kiasi gani bali ni unaamua nini unapozipata hizo pesa.  Unaweza amini kuwa mwenye kipato cha Tsh.300, 000 anajenga nyumba nzuri na mwenye Tsh.700, 000 anashindwa? Jibu ni rahisi na mifano mingi tunayo. Ushauri wangu kwako msomaji:

Unapopata fedha mikononi mwako, KWANZA tulia kabisa, pesa ni yako. Narudia tena, tulia kabisa kama vile huna hela. Baada ya kutuliza akili fanya yafuatayo. 

Hatua ya kwanza: Tenga kiasi cha AKIBA kwa ajili ya baadaye. Wataalamu wa masuala ya fedha hutumia neno "pay yourself first". Wakimaanisha jilipe mshahara wako kwanza. Akiba hii usiiguse kabisa ni kwa ajili ya baadaye. Save for yourself for rainy day. 

Jambo la pili: Tenga kiasi fulani kwa ajili ya KUWEKEZA. 
Kiasi hiki si akiba ni fedha unayoirundika polepole kwa ajili ya kukuza mtaji ili siku utakapohitaji kuanzisha biashara usihangaike sana. Kama unafuatilia uchumi wa dunia unavyokwenda utakuwa unafahamu kuwa kadri siku zinavyokwenda, upatikanaji wa mikopo utakuwa wa masharti sana. Hivyo ni jambo jema sana ukiweza kujijengea nidhamu ya kifedha ili tusitegemee mikopo tu kama chanzo cha mitaji wakati pesa zinazopita mikononi mwetu ni nyingi.

Jambo la tatu: Fedha inayobaki ndo iwe MATUMIZI YALIYO YA LAZIMA. 
Kumbuka kuna matumizi holela na matumizi yaliyo vipaumbele. Wengi tukipata fedha tunakimbilia kuweka kwanza matumizi ya kila siku, kisha ndo tunataka kuweka akiba kilichotuzidi. Hii inaweza kutumika kwa wale ambao walishajiweka vizuri kifedha. Kwetu sisi ambao bado tunaelekea kwenye mafanikio ni muhimu sana kufuata hizi kanuni za kifedha, financial management principles. 
NB: Sijasema mikopo ni mibaya la hasha! Mikopo ni mizuri ukiitumia vizuri.
 Muhtasari:
1. Weka akiba
2. Weka kiasi kwa ajili ya kuwekeza
3. Tenga matumizi yaliyo ya lazima. Kumbuka: Usiweke AKIBA kinachobaki. Haya niliyoyaandika yamenisaidia na mpaka leo nayatumia.
 Nawatakia mafanikio mema.

FEDHA ILIYO MKONONI MWAKO,