Ijumaa, 3 Machi 2017

Habari za asubuhi rafiki yangu!
Binafsi sijambo, namshukuru Mungu.
Leo nataka tujifunze namna ya kuchukua maamuzi sahihi tunapochukua MIKOPO (LOANS) katika kufanya biashara na matumizi mengine.

Ndugu msomaji wa mtandao huu; nina uhakika unajua kuwa mwanadamu maadamu yu hai hana budi anahitaji kuwa na fedha awe mkubwa au mdogo, awe tajiri au masikini, wote tunahitaji fedha. Huu ndio ukweli wa mambo.
Na katika uhitaji huu, uchumi wa dunia umekuwa ukijifunza na kufanya tafiti nyingi juu ya kuhakikisha kila mtu ili aweze kufanya biashara lazima ahitaji pesa au hela au fedha. Na kwa sababu hiyo, benki nyingi na taasisi mbalimbali duniani zimeanzisha mfumo wa kukopesha na kurudisha faida (riba) kwa aliyekukopesha fedha hizo (loan).

Ndugu rafiki yangu, shida imekuja pale wakopaji wanapojidanganya wakidhani mkopo ni msaada au huduma ya kusaidia wasiojiweza. Namaanisha nini?
Namaanisha kuwa unapokopeshwa fedha ujue aliyekukopa, anahitaji na RIBA katika fedha hiyo, upate hasara au upate faida lazima umrudishie fedha zake pamoja na RIBA. Na si kosa kumpatia RIBA mkopeshaji kwani anafanya biashara. 
Riba ni faida utakayomzalishia kwa kipindi maalumu mnachokubaliana kimkataba.
Nachotaka ufahamu ni hiki, aliyekukopa anafanya biashara na wewe, na ukiwa mzalishaji bora unakuwa mwaminifu kwa aliyekukopa.
Zingatia jambo hili: MKOPO ni BIASHARA.
Kwa kuwa siku hizi kumekuwa na ukosefu wa mitaji, taasisi mbalimbali za kifedha zilizo rasmi na zisizo rasmi zimeanzisha huduma za mikopo tena kwa urahisi zaidi, na kadri siku zinavyoendelea, huduma hii ya mikopo inazidi kupamba moto.
Na wahitaji kwa kutokujua hili, wamechangamkia FURSA hizi bila kujiuliza maswali, na hali zao za maisha wengine zimeyumba jumla. Sisemi kwa kukuogopesha, nasema ili ufanye maamuzi mazuri katika masuala ya mikopo.

Natamani nikushauri jambo moja kubwa! Siku zote unapochukua mkopo jiulize maswali yafuatayo:
1.Mkopo huu unatolewa na taasisi ipi?
Si watu wengi sana wanaotafuta mikopo wanajiuliza swali hili, wao wanachotaka ni hela tu, mengine baadaye! Kuwa mwangalifu juu ya hili. Unapotaka kukopa, fuatilia kutaka kujua hiyo taasisi ikoje. Ndiyo maana wengine wameumizwa jumla na wameporomoka kimaisha kwa sababu ya mahali walipochukua mikopo. Nakumbuka mwaka fulani, kuna taasisi walianzisha mfumo fulani, ukitaka mkopo, unatoa hela za kwako kwanza, wao wanakuambia kuwa, inabidi uwekeze kwanza kwao kisha baada ya muda wao watakukopesha fedha za kukutosha. Na kwa kuwa unakuwa na kiu ya fedha, unajikuta umetoa fedha zako. Ndugu msomaji, na mwaka huo watu wengi walitoa fedha zao na mpaka leo, hiyo taasisi ilikopotelea hakujulikani. 
Kumbuka kuwa, kuna uhusiano wa karibu kati ya fedha na hali ya kiroho ilikotoka fedha hiyo. Na hiyo roho itafuatilia hizo fedha. Ndiyo maana kuna sehemu ukikopa fedha huzifanyii chochote hata kama umejiandaa kufanya kitu fulani. Ukishazipata tu, akili inafanya kinyume, baada ya fedha kuisha ndipo unashtuka. Ikiwezekana unakopa tena na tena, mwisho wake, unaishia pabaya.
muhimu: Fanya uchunguzi wa kina wa mahali unataka kukopa fedha.

2. Unajua RIBA ya mkopo unaotaka kuchukua?
Ni muhimu na ni lazima uulize wahusika juu ya RIBA zao, na wanakokotoaje hizo riba. Waulize hizo riba ni kwa mwaka au kwa mwezi? Waulize usiwaogope, maana kuna wengine wakifika sehemu hizo utadhani wao ni malaika, waulize vizuri, ukiridhika sawa, usiporidhika achana nao, hiyo ni biashara sio huduma. Kwa mfano, unaweza ukaambiwa riba ni 1.6% , halafu wewe huulizi unajua riba nafuu. Au unafikiri nakutania? Wako watu wengi wamechukua mikopo bila kujua utaratibu wa riba.
muhimu: fahamu kwa undani utaratibu wa riba zao.

3. Je, naruhusiwa kufuta mkopo nje na muda tuliopatana?
Watu wengi hawaulizi swali hili muhimu sana, wao kwao kinachotafutwa ni fedha. Ndugu msomaji, waulize hivi: Naweza kuja kurudisha au kulipa fedha zenu hata kama ni kabala ya muda wa kimkataba? Waulize tena hivi: Mtu anapokuja kufuta mkopo wake, mnatoa riba au hamtoi? Na unapojibiwa waombe vipeperushi au maandiko yanayodhihirisha hayo. Usipende kuambiwaambiwa kwa mdomo tu. Omba kupewa nyaraka.
Lakini pia unaweza ukawauliza: Je, ikatokea nikafa, mkopo wangu utafutwa au waliobaki watawajibika nao? Omba kufafanuliwa vizuri. Kufa kupo maadamu unaishi chini ya jua.
Swali la mwisho, waulize hivi: Ikatokea nimekwama kifedha, naweza kusimamishiwa mkopo kwa muda fulani? Waulize wala usiogope!

4. Jiulize hili swali mwenyewe, "kwa nini nataka kuchukua mkopo?
Ndugu msomaji ni muhimu ujue jibu la swali hili, kwani mkopo ni fedha ya mtu amekupa uizalishe upate faida na mgawane hiyo faida. Ndiyo maana ni muhimu ujue kuwa mkopo ili uweze kumpatia faida yake mkopeshaji na wewe upate faida yako, huna budi kuizalisha. Kuna msingi mmoja wa fedha nao ni huu:Fedha huwakimbia wasiojua kuizalisha.
Usichukue mkopo kufanyia mambo ya ovyo hovyo wakati huna hata kitega uchumi kingine!
Wapo watu wanashangaza mno, wao ilimradi fedha zipo yeye atazichukua tu.

ushauri wangu kwako, usianze kuchukua mkopo mkubwa kwa mara ya kwanza, anza na kidogo ili ujue uwezo wako. Mkopo ni sawa na bunduki ya kuwindia wanyama, ukiitumia vizuri, unampata mnyama huyo, ukiitumia vibaya, unakugharimu wewe mwenyewe.

Nawatakia Jumamosi njema na baraka tele!
 

KWA NINI UNAHITAJI MKOPO?

POLENI WOTE KWA MAJUKUMU!
Mchana huu naomba ujiulize hili swali moja tu
Nifanye nini ili nitoke kwenye hii hatua ya maisha?

TAFUTA JIBU LA SWALI HILI MOJA TU

Alhamisi, 2 Machi 2017




MAFANIKIO NI KUWA NA VIPAUMBELE BORA

Email Address







Good evening my dear friends!
It's my hope that you are all fine.
Employability skills  are skills you need for a job.
For many people today, a career for life is no longer an option. Most people will hold jobs with a variety of employers and move across different employment sectors through their their working life.

         We all need to be flexible in our working working patterns and be prepared to change jobs and/ or sectors if we believe there are better opportunities elsewhere.

In order to be flexible we need a set of "transferable skills"- Skills that are not specific to one particular career path but are generic across all employment sectors.

The Job Skills Employers are Looking For
Employers are often looking for skills that go beyond qualifications and experience.
While your education and experience may make you eligible to apply for a job, to be successful in the role you will need to exhibit a mix of skills: "employability skills". 
This means that, the specialist, technical skills associated with different roles may be less important than the "soft skills" that can be transfered between different jobs and different sectors.
For many employers, getting the right people means identifying people with the right skills and qualities to fulfil the role and contribute to the organisation's success. Candidates may have the qualifications and "hard skills" needed to be able to manage the job role but, without a well-honed set of "soft skills", employers are less inclined to hire.

What are employability skills?
Those are skills necessary for getting, keeping and being successful in a job. They are the skills and attitudes that enable employyees to get along with their colleagues, to make critical decisions, solve problems, develop respect and ultimately become strong ambassadors for the organization.
Employment or "soft skills" are the foundation of your career building blocks and they are frequently referenced in the media as lacking in school-leavers, graduates and those already in employment (in-service).
Organisations spend a lot of money and time training staff, not in job specific areas but in general and basic skills.
NOTE: In times of high unemployment, employers have more choice of applicants and will favor those with well-rounded employability skills.
Keep in mind:
Different roles require different skill sets and abilities.
Here at VIPAUMBELEKWANZA there will forthcome a series of skills you need to help you get a job. The series are:
1. Writing a CV
2. Applying for a Job
3. Writing a covering Letter
4. Writing an effective Linked in profile
5. Interview Skills.
May you be blessed, yours author Faustin Mahende. 

EMLOYABILITY SKILLS

Jumatano, 1 Machi 2017

Habari za Alhamisi ndugu msomaji wa VIPAUMBELA KWANZA! 
Natumaini unaendelea vizuri katika harakati za kupambana na maisha ili uweze kufanikiwa. Ndugu msomaji wa makala zangu, kuna kitu watu wengi wamesahau kukifanya na kinawagharimu mno. Si mara nyingi watu huwa tunajitathmini kwa nini tunakwama kila siku katika kufanikisha ndoto (vision) zetu tulizonazo.
Umewahi kujiuliza kwa nini unakwama kila wakati? 
Umewahi kukaa chini angalau muda wa hata nusu saa ili utafakari kwa nini huvuki mahali ulipo kimaisha? Wengi tukikwama huwa tunakimbilia kuwalaumu wengine, hutaona tukijilaumu na kujitathmini sisi wenyewe kwanza; na hii imetufilisi fikra zetu na mitazamo ya kimaisha tuliyo nayo (mindset).
Ulishawahi kujiuliza haya maswali? Nadhani umewahi kujiuliza. Na kama hujajiuliza leo nakushauri kaa chini ujiulize hayo maswali.
Laiti watu wengi tungekuwa na tabia ya kujifunza kutokana na makosa tunayofanya tungekuwa mbali sana kimaendeleo.
Leo nataka nikupe ushuhuda wa kwangu binafsi ulionisaidia nikaanza kuvuka baadhi ya maeneo, si kwamba nimekwisha kufika, bado napambana kama wewe, ndio maana nakushirikisha ili tupambane wote kuelekea kwenye maendele na mafanikio ya maisha yetu. Unajua dunia hii ina FALSAFA nyingi sana, nyingine zinatusaidia nyingine hazitusaidii. Ni uamuzi wako ufuate "phillosophy" ipi katika maisha yako kwa kuwa maisha ni uchaguzi.

ushuhuda

Mwaka 2013 ni mwaka nimeanza kazi katika taasisi fulani hapa nchini. Nimeanza kazi hiyo pamoja na marafiki zangu kama tano (5) hivi. Nilipoanza kazi nilikuwa na malengo mengi sana na nilijua ndo nimefanikiwa kimaisha jumla. 
Maisha yaliendelea, na baada ya muda nilianza kupigiwa simu za ndugu na marafiki wakihitaji msaada wa kipesa, na mimi sikuona shaka kuwapa wakati NAJIONA kuwa fedha ninazo japo hazikuwa nyingi. Na ndugu hawa baada ya kuona wakiomba msaada kwangu hawanyimwi waliamua kunitegemea jumla bila ya mimi kujua. Baada ya mwaka mmoja na miezi kadhaa, nilianza kuingia kwenye madeni ya hapa na pale. Kilichonifanya nikajikuta kwenye madeni ni huruma zangu za kuwaokoa ndugu zangu waliokuwa wakihitaji msaada kwangu kifedha.
Maisha yalizidi kuwa magumu hata ikafika mahali nikaaanza kukata tamaa na ndoto zangu. Wakati huo nilikuwa na mchumba au rafiki wa kike niliyekuwa nimemuahidi kumuo siku si nyingi. Ghafla, ugomvi ulianza baina yangu na yeye, hii ilitokana na yeye kuona kuwa nampa ahadi hewa, na hii ni KWA SABABU SIKUMWAMBIA UKWELI KUHUSU hali niliyokuwa nayo. 
Siku moja huyo mchumba wangu alinipigia simu usiku. akaniuliza hivi: Faustine! do you really need me to be your wife? Nilimjibu , yes my dear, I do!
Ndipo aliponiuliza hivi, mbona nikikuomba hela hata elfu 10 unaniambia subiri mwisho wa mwezi? Aliongeza tena akasema, kwani kuna shida gani, ni kweli hela huna au una binti mwingine?
 Aliendelea kunilaumu sana, na wakati huo nilikuwa napigiwa simu nyumbani kwa kila tatizo lililojitokeza hata kama lilikuwa ndani ya uwezo wao. Madeni yaliendelea kunitesa nikafika mahali hta kukopa siwezi tena. Ndipo nilipoona kuwa maisha yamenishinda, japo kwa nje niliokena ninazo pesa.
Baada ya miaka 2na miezi hivi, nilikuwa hata siwezi kumudu hata kula chakula cha kushiba, nikaona sasa naelekea kufa.
Tarehe 25 ya mwezi Disemba 2015 nikiwa nasherehekea "KRISMASI" lilikuja swali moyoni mwangu, nalo lilikuwa hivi: Nitaishi maisha haya mpaka lini na huku nina AJIRA? Nikajiuliza tena, " kwa nini nisiwashirikishe wazazi wangu, na watu wa karibu kwangu juu ya hali niliyo nayo? 
Nikaamua kuwashirikisha wazazi wangu kuhusu madeni na hali niliyonayo. Nilimshirikisha pia mchumba wangu hali niliyokuwa nayo japo kwa aibu.
Wazazi wakaniambia hivi, unajua kwa nini umekwama kimaisha? Nikajibu ndiyo! Baba akaniuliza, ni nini? Nikamwambia "nina wategemezi wengi". Baba akasema "hapana". Tatizo ni wewe mwenyewe!
Alivyosema hiyo sentensi nilifikiria sana kwa nini amesema hivyo.
Ghafla nikagundua jambo lifuatalo ambalo lilibadilisha maisha yangu.
1. Niligundua kuwa nilidhani kwa kuwa ninapata pesa kila mwezi, basi nitafanikiwa.
2. Niligundua kuwa huwa sijifikirii KWANZA kabla ya kuwafikiria wengine.
3. Niligundua kuwa kila hela ndogo ninayoipata ni ya muhimu kwangu.
4. Nilifahamu kuwa, nilitakiwa nijikwamue kwanza mimi ndipo nianze kuwasaidia ndugu zangu.
5. Niligundua kuwa hata fungu la kumi si mtoaji kabisa.

UAMUZI NILIOCHUKUA.
1. Niliamua kuomba toba kwa Mungu juu ya matumizi yangu ya fedha.
2. Nilitengeneza mfumo wa kifedha wa "kuweka akiba kila mwezi " KABLA ya kupanga matumizi ya pesa.
3. Nilianza kuweka vipaumbele katika maisha yangu na kuvitendea kazi.
4. Nilianza kuwekeza pesa nyingine.
5. Nilianza kuishi uhalisia wa maisha yangu.
6.Nilianzisha chanzo kingine cha kipato nje na AJIRA, na hapa ndipo nilipoanza kufurahia maisha kwa kiasi fulani.
Ndugu msomaji, naomba nikushauri mambo yafuatayo:
1. Usiishi jinsi usivyo ili kuwafurahisha wanaokutazama, maana mafanikio yako, yako mikononi mwako.

2.Jizoeze kuweka akiba kwa kila fedha unayopata hata kama ni ndogo.

3 .Usianze kuwabeba wategemezi ulionao wakati bado na wewe umenaswa. Waeleze ukweli kuwa bado kuna mambo unayaweka sawa. Msema kweli ni mpenzi wa Mungu japo ukweli haupendwi na wengi.

4. Epuka madeni, na kama unayo yalipe kwanza hata kidogo kidogo. Hutaweza kufanikiwa na kuwa huru wakati bado ni mdaiwa. LIPA DENI ULIZO NAZO, waeleze ukweli wanaokudai kuwa utaanza kuwalipa, usiwakimbie kawaeleze ukweli wa maisha yako, nao ni binadamu, watakupa utaratibu wa jinsi utakavyowalipa. DAWA YA DENI NI KULILIPA si zaidi ya hapo.

5. ANZISHA BIASHARA AU CHANZO CHA KIPATO kingine.

6. Amua kuwa utabadilika katika maisha yako, na hapo ndipo utakapoweza kuona mafanikio yako.


Mungu awabariki, wako MASTER WA VIPAUMBELE KWANZA.

 

JIFUNZE KUTOKANA NA MAKOSA ULIYOFANYA

Jumamosi, 25 Februari 2017

Habari za usiku ndugu msomaji wa VIPAUMBELE KWANZA.
Naomba tushirikiane kujibu hili swali. Nalo ni:
"Kwa nini sina biashara yoyote? Ndugu msomaji huwa nashangaa kila wakati watu wanapokuwa wanalalamika eti wameshindwa kufanya biashara. Unajiuliza kwa nini, unakosa majibu. Kuna rafiki yangu alikuja nyumbani napoishi tulipokuwa tunazungumza, aliniuliza swali lifuatalo ambalo naamini huenda na wewe linakusumbua. Swali nililoulizwa liko hivi:
"Ni biashara gani inayolipa zaidi"? Je, ungekuwa ni wewe umeuliza ungemjibuje?
Nilielewa ghafla kuwa huyu ndugu anafikiri kuwa ili ufanikiwe kuna biashara fulani unayotakiwa kufanya. Niliendelea kuzungumza naye mambo kadhaa yahusuyo maisha.

Kwa nini kila siku hili swali huulizwa? why?
Umefika wakati wa sisi kwa sisi kuelezana ukweli..
Ndugu msomaji wa hii makala, kiukweli hakuna BIASHARA nzuri kuliko zote, kwa sababu biashara ili ifanikiwe inategemea mambo mengi kama vile
  • Eneo biashara ilipo
  • Usimamizi wa biashara
  • Mtaji wa biasha
  • Uhitajiwa wa biashara.
Yapo mambo mengi sana yanayochangia biashara kukua na kufanikiwa. Unaweza ukaanza biashara ya fedha nyingi na bado usifanikiwe kama ulivyotarajia.
Hebu tujibu swali hili linaloulizwa kila siku:
KILA BIASHARA INALIPA NA KILA BIASHARA INAWEZA ISILIPE
Watu wanaouliza hili swali tatizo lao ni hofu ya kufilisika, na wengine hawana mitaji ya kuanzisha biashara. Wengi ni waoga kuanzisha biashara. Hasa wale walioajiriwa, na hii ni kutokana na elimu dunia ilivyowazoesha kulipwa, ni waoga kuthubutu. Ndugu msomaji, mafanikio yako mikononi mwako, ukiona unaogopa kuthubutu, ikiwezekana, mwombe Mungu akusaidie. 

La pili ni kutokuwa na mitaji.
Huwa siamini kuwa watu hawana MITAJI ya kuanzisha biashara. Kama ni kweli hawana, yafuatayo hujitokeza, nayo ni: 
1.Wanataka kuanza na biashara kubwa kubwa, kitu ambacho kinawachukua muda mrefu sana.
2. Au hawako serious na biashara. Kwa sababu mtu mwenye kipato cha sh.5000 kwa siku hawezi kusema hana mtaji, ni kutokuwa na matumizi mazuri ya fedha anazopata. Niliwahi kushuhudia, mtu akianza biashara kwa sh.15000 tu. Huwezi amini lakini nilishuhudia. Shida ni fikra zetu, tunataka tuwe mamilionea ndani ya siku 14, haiwezekani ndugu yangu. Anza na kidogo, uwe na uhakika utafika unakotaka kwenda.

Ukiona mtaji hakuna, kusanya nguvu na wenzako mfanye biashara kwa pamoja. Muhimu mnaoshirikiana nao wawe waaminifu na uwe mwangalifu sana. Maana biashara ya kikundi si mara nyingi mwisho wao ni mzuri. Lakini wapo wanaofikia malengo yao..

Tatu unaweza ukakopa ikiwezekana, lakini usiwe mwepesi sana kuchukua mikopo ilimradi inapatikana. Kama huna uhakika na unachotaka kuufanyia huo mkopo, usichukue maana utakugharimu.

Tukijaliwa, nitakuja kuelezea vitu vya kuzingatia unapochukua MKOPO, na maswali unayopaswa kujiuliza kabla hujachukua MKOPO.
Nikutakie usiku mwema! 
   

KWA NINI HUNA BIASHARA?

Habari za jioni ndugu msomaji! Pole kwa majukumu ya hapa na pale. Mshukuru Mungu kwa yote yaliyotukia yawe mazuri au mabaya.
Jioni napenda nikushirikishe jambo hili muhimu japo wengi wanaliona kama halina umuhimu. Jizoeze kuwafundisha au kuwapa maarifa watoto wako yatakayowasaidia siku za usoni. Sizungumzii elimu dunia iliyo katika mfumo rasmi, hapana nazungumzia maarifa. Watu wengi wanafikiri wataishi milele, na kwa sababu hiyo kuna baadhi ya vitu huwa wanavipuuzia katika maisha yao.

Katika jioni njema nakushauri jizoeze kukaa na watoto wako mara kwa mara, kama wako shule iwe day au boarding (bweni) bado watakuja nyumbani likizo! Kama wewe ni mfuatiliaji wa mambo utagundua kuwa watoto wetu wanahitaji kupata vitu hivi katika maisha yao! Ukifa haya mambo yatawasaidia sana, ndiyo maana haijalishi mtaacha mali nyingi kiasi gani, kama hawakuandaliwa uwe na uhakika mali zitaisha na hawatazifaidi kabisa. Ni mambo tunaona kila siku.

Mambo hayo ni:
1. Lazima watoto wako wafundishwe masuala ya fedha
2. Lazima wajifunze kompyuta ipasavyo
3. Lazima wawe na hofu ya Mungu maishani mwao.
 Kila upatapo mwanya wafundishe watoto wako mambo haya yatawasaidia sana pindi hampo. Hakuna atakayeishi milele, kila mwenye mwili hana budi atatoka katika dunia hii.

FEDHA ni nguzo ya muhimu sana kwa kila mtu kujifunza ili itumike ipasavyo.
Ni muhimu wanao wajue tabia za fedha na misingi yake, kwani jambo hili litawasaidia. Jambo hili sio OPTIONAL (si la kuamua uchague au usichague), ni lazima wajifunze vema. Fedha zimeangamiza wengi sana hata watu wazima tena wenye elimu. Kibaya zaidi hiki kitu cha fedha, hutakikuta kwenye SYLABUS ya mfumo wa elimu wa nchi yetu. Kuna watu ni maskini kwa kuwa tu walikosa kujua TABIA ZA FEDHA. Usiishie tu kuwapeleka shule ukadhani umemaliza, wafundishe kila wakati. Kwa mfano, jizoeze kuwapa hela za matumizi na baadaye waulize wamezitumiaje. Wafundishe kujua vitu ambavyo ni VIPAUMBELE kwao na VILE ambavyo sio VIPAUMBELE kwao. Watu wengi wamefaulu kuweza kutafuta fedha, wengi wanakwama kwa kuwa hawajui namna ya kukaa nazo hizo fedha. Siku moja nilikuwa namfundisha mdogo wangu namna ya kukaa na fedha kwa nidhamu, nikamuambia hivi, siku zote, ukipata fedha iwe ndogo au kubwa lazima kabla ya matumizi, atoe FUNGU LA KUMI, baada ya fungu la kumi, ajilipe yeye au aweke AKIBA. Baada ya akiba, atenge kiasi cha KUWEKEZA. Na pesa itakayobaki iwe ni MATUMIZI YALIYO LAZIMA. Mfundishe mengi hatua kwa hatua, hatakusahau. Mpaka hivi tunavyoongea, mdogo wangu ananishukuru kwa jambo hili.

KUJUA KOMPYUTA SI UCHAGUZI
Siku tulizo nazo ni za TEKINOLOJIA (technology), hivyo awe amepata elimu dunia au awe hajapata elimu dunia, lazima mtoto katika nyakati hizi ajue kutumia kompyuta. Awe maskini au awe tajiri, computer lazima ajifunze...
Tutafiki wakati mambo mengi tunayoyaona leo yakifanyika kikawaida yatakuwa kitekinolojia zaidi. Uwe mfanyabiashara mdogo au mkubwa na hujapata elimu dunia, lazima ujifunze na wewe kutumia computer na pia lazima wanao wajue kutumia hiki kifaa muhimu cha kielektroniki. Miaka mingi iliyo mbele yetu utajua jambo hili ninalokueleza. Nakuomba uyafanyie kazi.

KUWA NA HOFU YA MUNGU
Ewe mzazi wa kizazi hiki nadhani huhitaji kushawishiwa kumlea mwanao katika njia impasayo ili baadaye awe baraka kwa jamii na kwa dunia. Siku hizi kuna mambo mengi yanayojitokeza tena mengine yanakubaliwa kisheria, hivyo watoto wetu tuliopewa tuhakikishe tunawapa malezi bora kila wakati. Siku hizi kuna USHOGA, na mambo yanayofanana na hayo, tujitahidi kuwaonya kwa huzuni na kwa uchungu, huku tukiwaeleza mabaya haya lakini la muhimu zaidi kuwafundisha kumjua Mungu na kumtumikia yeye. Tukipoteza watoto tumepoteza jamii na ulimwengu. Watoto wetu wanazaliwa katika nyakati hizi mbaya. Mungu awe nawe, nakutakia jioni njema. Wako VIPAUMBELEKWANZA master!
 

VITU HIVI VINNE AMBAVYO HUNA BUDI KUWAFUNDISHA WATOTO WAKO

Ijumaa, 24 Februari 2017

Ndugu msomaji wa VIPAUMBELE KWANZA umeamkaje siku ya leo? Ni matumaini yangu kuwa umeamka mapema kabisa na harakati za kupambana na maisha ya kila siku. Leo hii napenda nikushirikishe jambo moja muhimu. 
Je! umejiandaa vya kutosha kuishi katika mafanikio ya kiuchumi miaka 5 ijayo yaani 2023. Umejiwekea malengo gani ya kuhakikisha unakuwa na uchumi mzuri kufikia mwaka 2023? Siku moja nilimuuliza hili swali rafiki yangu nayefanya naye kazi mahali fulani akaniambia hivi, "Faustine huwezi kuweka malengo ya miaka mingi hivo, akaendelea kusema, "una uhakika gani kuwa mwaka 2023 utakuwa hai? Mimi kwanza nilimshangaa na nilishtuka sana, nilitegemea angeniambia, ondoa mashaka. Huu ndio ukweli halisi, watu wengi hasa vijana wa kizazi hiki, kweli wanatafuta fedha na wanapata, cha ajabu mno, wanazitumia ovyo hovyo, mwisho wa siku wanajikuta hawana kitu. Wengi wanajitahidi wananunua mashamba na viwanja ni vizuri sana. Lakini swali langu liko pale pale, wamejiandaaje kifedha miaka hiyo ijayo? Ndugu msomaji unayesoma makala hii, inawezekana umeshajijenga, Mungu akuinue zaidi, lakini pia inawezekana bado unapambana, ningekushauri ujitahidi kuwa na malengo mahususi ya kimkakati na yanayotekelezeka. Ili uweze kujiandaa vizuri fanya jambo hili moja tu kwanza.
ANZA KUWEKEZA FEDHA ZAKO KIDOGO KIDOGO .
Narudia tena anza kuwekeza fedha zako kidogo kidogo kwa watoao riba. Nina uhakika baada ya muda utaanza kuona mafanikio kwako. Ngoja nikupe mfano mzuri.
Kuna rafiki yangu mmoja alinitangulia kikazi, yeye alivyoanza kazi yake alipata bahati ya kuwa na siri hii muhimu. Akatafuta taasisi nzuri akawekeza fedha zake kwa miaka 5 tu. Alijinyima akaanza kuweka (deposit) Tsh.50,000 kila mwezi kwa miezi 60 au miaka 5. Akajikuta ana Tsh.499,645.19 ambayo ukikadiria ni karibu Sh.5, 000, 000. Akapata mtaji wa kuanzia biashara. Hivi leo tunavyoongea yuko mbali kimaisha. Unaweza ukasema, anafanya kazi, ni sawa, lakini ukipiga mahesabu yako vizuri utagundua kuwa, sh.50, 000 kwa mwezi ni sawa na sh.1300 kwa siku. Ubaya ni kwamba, vijana walio wengi siku hizi wanatumia fedha zao kwa fujo wakidhani kuwa wataendelea kuwa nazo. Si kweli usijidanganye, maisha yanabadilika, miili yetu inachoka. Ifike mahali fedha nazo zitufanyie kazi. Unataka kuniambia huwezi pata sh. 1000 tu kwa siku ukaiweka kando? Kama huwezi angalia unatumia shilingi ngapi kwenye vocha ya simu na mawasiliano kwa mwezi. Nakushauri jitahidi usiishi kama BOSS wakati bado hujafikia uhuru wa kutosha wa kifedha. Acha kutapanya pesa, kumbuka una wategemezi wengi hapo baadaye. Na kama tayari unao wategemezi, basi huna budi kutulia na kujipanga vema. 
Ndugu msomaji, mwaka juzi kuna kundi la watu 7 waliungana wakawa wanaungana kwa kuweka sh. 50,000 kila mwezi kila mmoja. Hivyo wanachanga sh.350, 000 na wameamua kufungua biashara fulani mwaka 2021, kwa mahesabu ya haraka hawatakosa mil.48. Hii ni nguvu ya uwekezaji. Nakutakia siku njema! 

UMEJIAANDAJE KIUCHUMI MIAKA 5 IJAYO?